Yoshua 19 SWHULB
Yoshua Chapter 19 SWHULB Bible Verse Images
Copyright © 2019 Door43 World Missions Community
Language: Kiswahili (Swahili)
Translation by: Door43 World Missions Community
Contributors: Alfred Danjuma, Bariki Malisa, Christina Abraham Kileo, Cloud Roman, Daniel Marura Chacha, Dina Mast, Dina Roman, Donald Shadarck Dutuyi, Emmanuel Masanja Mbaaga, Emmanuel Nyamalya, Erasmus Peter Malelo, Ev. Lazaro Chalomhola, Ezekiel Manala, Fred, Gabriel Gidale Merus, Gabriel Lwitakubi Mazige, James Makula, James Semnkai, Jeremiah Masasi, Jesse Katabi Masolwa, John Ojasi, Joyce Gilbert Masasi, Karen Riecks, Kazwanomo, Kennedy, Ker, Lameck Yakobo Tobotobo, Laurent Petro Malelo, Lazarus David Chalomhola, Makene Mafwele, Marco Luma Mahushi, Mathew Nkusa, Mathias William, Mr. James Semnkai .It., Musa Isaya Majama, Musa Luzali, Pastor John Kerim, Pastor Jordan, Philipo Mussa Kanwelle, Raphael Musa, Rev. Charles Mabisa, Rev. Yohana Batano, Robert Ndalahwa, Sadiki Kulwa, Samson Nungwana, Thobias Kazwanomo, Yohana Dutuyi, Yohana Magera, Zelote Loilang'akaki Lukumay, Rev. Erasmus Peter Malelo, Ev. Mathew Kazimoto, Rev. Dr. David Magoke, Rev. Elias Ndema, Rev. Alex Nyuri, Rev. Gungutu Elias, Rev. Lameck Tobotobo, Rev. Catherin D. Matia, Rev. Yohana S Dutuyi, Rev. Donald Dutuyi, GS. Andrew Gewe, Ev. Ezekiel Daudi, Rev. John Ndaluka, Ev. Moses Malugu, Rev. Moses Eliakim Ndege, Past. Isack A. Gomugo, Past. Mathias William, Rev. Yekonia M. Koko, Rev. Elisande Mhanga, Ev. James A. Makula.
This translation is made available to you under the terms of the Creative Commons Attribution Share-Alike license 4.0.
You have permission to share and redistribute this Bible translation in any format and to make reasonable revisions and adaptations of this translation, provided that:
- You include the above copyright and source information.
- If you make any changes to the text, you must indicate that you did so in a way that makes it clear that the original licensor is not necessarily endorsing your changes.
- If you redistribute this text, you must distribute your contributions under the same license as the original.
Credits: In addition, we would like to give very special thanks to eBible.org for making Swahili Unlocked Literal Bible available in MySQL format.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Upigaji wa pili wa kura uliangukia kwa Simoni na waligawiwa kwa kila ukoo wao. Urithi wao ulikuwa katikati ya urithi ulikuwa ni mali ya kabila la Yuda.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Urithi waliokuwa nao ni Beerisheba, Sheba, Molada,
Square Portrait Landscape 4K UHD
Simoni alikuwa pia na Ziklagi, Bethi Markabothi, Hazari Susa,
Square Portrait Landscape 4K UHD
Bethi Lebaothi, na Sharuheni. Kulikuwa na miji kumi na mitatu pamoja na vijiji vyake. Vile vile
Square Portrait Landscape 4K UHD
Simoni alimiliki Aini, Rimon, Etheri, na Ashani. Hii ilikuwa ni miji minne pamoja na vijiji vyake.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Miji hii pamoja na vijiji vilivyoizunguka hata kufika Baalathi Beeri (ambao ndio Rama katika Negevu). Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Simoni, waliopewa kwa koo zao.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Urithi wa kabila la Simoni ulikuwa sehemu ya himaya ya kabila la Yuda. Hii ni kwasababu nchi waliyopewa kabila la Yuda ilikuwa ni kubwa kwao, na hivyo kabila la Simoni lilipokea urithi wao kutoka katika sehemu yao ya katikati.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Upigaji wa kura ya tatu uliangukia kwa kabila la Zabuloni, na walipewa kwa koo zao. Mpaka wa urithi wao ulianzia huko Saridi.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mpaka wao ulipanda upande wa magharibi kuelekea Marala na ukaigusa Dabeshethi, na kisha ukasonga kuelekea kijito kilichokuwa mkabala na Yokineamu.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kutoka Saridi mpaka ulizunguka upande wa mashariki kuelekea mashariki na ulienda hadi mpaka wa Kislothi Tabori. Kutoka hapo uliendelea hadi Daberathi na kisha ulipanda hata Yafia.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kutoka hapo ulipita katika upande wa mashariki mwa Gathi Heferi, na kisha ukafika Ethikazini, baadaye ulienda hadi Rimoni na kisha ukageuka kuelekea Nea.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mpaka ulizunguka kueleka kaskazini ukafika Hanathoni na ulikomea katika bonde la Ifta Eli.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mkoa huu ulijumuisha miji ya Katathi, Nahalali, Shimroni, Idala, na Bethlehemu. Kulikuwa na miji kumi na miwili, pamoja na vijiji vyake.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Zabuloni, waliopewa kwa kufuatana na koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Upigaji kura wa nne uliangukia kwa Isakari, na waligawiwa kufuatana na koo zao.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Eneo lao lilijumuisha Jezreelli, Kesuloothi, Shunemu,
Square Portrait Landscape 4K UHD
Pia ilijumuisha miji ya Rabithi, Kishioni, Ebezi,
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mpaka wao ulifika Tabor, Shahazuma, na Bethi Shemeshi, na ukakomea katika Yordani. Ilikuwa ni miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Isakari, na walipewa kufuatana na koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Upigaji wa kura ya tano uliangukia kwa kabila la Asheri, na walipewa kwa koo zao.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Eneo lao lilijumuisha miji ya Helikathi, Hali, Beteni, Akashafu,
Square Portrait Landscape 4K UHD
Alameleki, Amadi, na Mshali. Mpaka wa magharibi ulitanuka hadi Karmeli na Shihori Libnathi.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha ulizunguka upande wa mashariki kueleka Bethi Dagoni na ukaenda hadi Zabuloni, na kisha ukafika katika bonde la ifutaheli, upande wa kaskazini mwa Bethemeki na Neieli. Baadaye uliendelea mbele hata Kabuli kueleka upande wa Kaskazini.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Na kisha ulienda hadi Ebroni, Rehobu, Hammoni, na Kana, hata kufika mji mkubwa wa Sidoni.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mpaka ulirudi nyuma kuelekea Rama, na kisha ukafika kwenye mji wa Tiro uliokuwa na ngome. Baada ya hapo mpaka ulizunguka kuelekea Hosa na ulikomea katika bahari, katika mkoa wa Akizibu,
Square Portrait Landscape 4K UHD
Umma, Afeki, na Rehobu. Kulikuwa na miji ishirini na miwili, pamoja na vijiji vyake.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Asheri, na waliopewa kwa koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Upigaji wa kura wa mara ya sita uliangukia kwa kabila la Nafutali, na walipewa kufuatana na koo zao.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mpaka wao ulianzia Helefu, kutoka katika mwaloni huko Zaananimu, ulipanda hadi Adaminekebu na Yabneeli, umbali kama Lakumu; na ulikomea katka Yordani.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mpaka ule ulizunguka upande wa magharibi kuelekea Aznothi Tabori na ulipanda hadi Hukoki; uligusa Zabuloni katika upande wa kusini, na ulifika hata Asheri katika upande wa magharibi, na Yuda katika upande wa mashariki huko katika mto Yordani.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Miji yenye ngome ilikuwa ni Zidimu, Zeri, Hammathi, Rakathi, Kinnerethi,
Square Portrait Landscape 4K UHD
Pia kulikuwa na miji ya Yironi, Migdaleli, Horemu, Bethi Anathi, na Bethi Shemeshi. Kulikuwa na miji kumi na tisa, pamoja na vijiji vyake.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Nafutali, na walipewa miji pamoja na vijiji vyake kufuatana na koo zao.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Upigaji wa kura ya saba uliangukia kwa kabila la Dani, na walipewa kufuatana na koo zao.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Eneo lao la urithi lilijumuisha miji ya Zora, Eshitaoli, Iri Shemeshi,
Square Portrait Landscape 4K UHD
Vile vile lilijumuisha miji ya Eloni, Timna, Ekroni,
Square Portrait Landscape 4K UHD
Me -Yarkoni, na Rakoni sambamba na eneo la karibu na Yopa.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ilitokea wakati mpaka wa kabila la Dani ulipowapotea, kabila la Dani waliishambulia Leshemu, wakapigana nao, na wakauteka. Waliua kila mtu kwa upanga, wakauchukua ukawa mali yao, na wakakaa ndani yake. Wakauita mji ule Dani jina la babu yao badala ya Leshemu.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Huu ulikuwa urithi wa kabila la Dani, waliopewa kufuatana na koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Walipomaliza kugawana urithi wa nchi, watu wa Israeli walimpa urithi Yoshua mwana wa Nuni kutoka miongoni mwao.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa amri ya Yahweh walimpatia mji wa Timnathi Sera ambao aliuomba, ulikuwa katika nchi ya milima ya Efraimu. Aliujenga mji na akaishi huko.
Square Portrait Landscape 4K UHD
Na huu ndio urithi ambao Eliazari kuhani, na Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa makabila ya familia za mababu zao miongoni mwa watu wa Israeli, waligawa kwa kupiga kura huko Shilo, mbele za Yahweh katika mlango wa hema la kukutania. Na hivyo wakamaliza kuigawa nchi.
Available Bible Translations
Joshua 19 (ASV) »
Joshua 19 (KJV) »
Joshua 19 (GW) »
Joshua 19 (BSB) »
Joshua 19 (WEB) »
Josué 19 (LSG) »
Josua 19 (LUTH1912) »
यहोशू 19 (HINIRV) »
ਯਸ਼ਵਾ 19 (PANIRV) »
যিহোচূৱা 19 (BENIRV) »
யோசுவா 19 (TAMIRV) »
यहोशवा 19 (MARIRV) »
యెహోషువ 19 (TELIRV) »
યહોશુઆ 19 (GUJIRV) »
ಯೆಹೋಶುವನು 19 (KANIRV) »
يَشُوع 19 (AVD) »
יהושע 19 (HEB) »
Joshua 19 (BSL) »
Giô-sua 19 (VIE) »
Josué 19 (RVA) »
Giosué 19 (RIV) »
约 书 亚 记 19 (CUVS) »
約 書 亞 記 19 (CUVT) »
Jozueu 19 (ALB) »
Josua 19 (SV1917) »
Иисус Навин 19 (RUSV) »
Ісус Навин 19 (UKR) »
Józsué 19 (KAR) »
Исус Навиев 19 (BULG) »
ヨシュア記 19 (JPN) »
Josvas 19 (NORSK) »
Jozuego 19 (POLUBG) »
Yashuuca 19 (SOM) »
Jozua 19 (NLD) »
Josua 19 (DA1871) »