1 Samweli Chapter 20 SWHULB Bible Verse Images

1 Samweli 20 Bible Verse Pictures. Choose from a large collection of inspirational, motivational and encouraging Bible verses with pictures of nature. Download and share 1 Samweli 20 inspirational Bible verse images. Bible verse pictures were created based on verses from the Swahili Unlocked Literal Bible (SWHULB). The Holy Bible in the Swahili language, Unlocked Literal Bible version.

Copyright © 2019 Door43 World Missions Community
Language: Kiswahili (Swahili)
Translation by: Door43 World Missions Community

Contributors: Alfred Danjuma, Bariki Malisa, Christina Abraham Kileo, Cloud Roman, Daniel Marura Chacha, Dina Mast, Dina Roman, Donald Shadarck Dutuyi, Emmanuel Masanja Mbaaga, Emmanuel Nyamalya, Erasmus Peter Malelo, Ev. Lazaro Chalomhola, Ezekiel Manala, Fred, Gabriel Gidale Merus, Gabriel Lwitakubi Mazige, James Makula, James Semnkai, Jeremiah Masasi, Jesse Katabi Masolwa, John Ojasi, Joyce Gilbert Masasi, Karen Riecks, Kazwanomo, Kennedy, Ker, Lameck Yakobo Tobotobo, Laurent Petro Malelo, Lazarus David Chalomhola, Makene Mafwele, Marco Luma Mahushi, Mathew Nkusa, Mathias William, Mr. James Semnkai .It., Musa Isaya Majama, Musa Luzali, Pastor John Kerim, Pastor Jordan, Philipo Mussa Kanwelle, Raphael Musa, Rev. Charles Mabisa, Rev. Yohana Batano, Robert Ndalahwa, Sadiki Kulwa, Samson Nungwana, Thobias Kazwanomo, Yohana Dutuyi, Yohana Magera, Zelote Loilang'akaki Lukumay, Rev. Erasmus Peter Malelo, Ev. Mathew Kazimoto, Rev. Dr. David Magoke, Rev. Elias Ndema, Rev. Alex Nyuri, Rev. Gungutu Elias, Rev. Lameck Tobotobo, Rev. Catherin D. Matia, Rev. Yohana S Dutuyi, Rev. Donald Dutuyi, GS. Andrew Gewe, Ev. Ezekiel Daudi, Rev. John Ndaluka, Ev. Moses Malugu, Rev. Moses Eliakim Ndege, Past. Isack A. Gomugo, Past. Mathias William, Rev. Yekonia M. Koko, Rev. Elisande Mhanga, Ev. James A. Makula.

This translation is made available to you under the terms of the Creative Commons Attribution Share-Alike license 4.0.

You have permission to share and redistribute this Bible translation in any format and to make reasonable revisions and adaptations of this translation, provided that:

  • You include the above copyright and source information.
  • If you make any changes to the text, you must indicate that you did so in a way that makes it clear that the original licensor is not necessarily endorsing your changes.
  • If you redistribute this text, you must distribute your contributions under the same license as the original.

Credits: In addition, we would like to give very special thanks to eBible.org for making Swahili Unlocked Literal Bible available in MySQL format.


1 Samweli 20:1 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha Daudi akakimbia kutoka Nayothi huko Rama akaenda na kumwambia Yonathani, “Nimefanya nini? Uovu wangu ni upi? Dhambi yangu ni ipi kwa baba yako, inayofanya atafute kuutoa uhai wangu.”

1 Samweli 20:2 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yonathani akamwambia Daudi, “La hasha; hautakufa. Baba yangu hafanyi jambo kubwa wala dogo bila kunijulisha. Kwa nini inamlazimu baba yangu anifiche jambo hili? La, siyo hivyo?”

1 Samweli 20:3 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Bado Daudi aliapa tena na akasema, “Baba yako anajua wazi kwamba nimepata kibali machoni pako. Pengine anasema, 'Asije Yonathani akajua jambo hili, labda atahuzunika.' Lakini kweli kama BWANA aishivyo, kama wewe uishivyo, kuna hatua moja tu kati yangu na mauti.”

1 Samweli 20:4 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha Yonathani akamwambia Daudi, “Lolote utakalosema, nitakufanyia.”

1 Samweli 20:5 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Daudi akamwambia Yonathani, “Kesho ni siku ya mwezi mpya, na inanibidi kukaa na kula pamoja na mfalme. Lakini acha niende, ili niweze kujificha katika shamba hadi siku ya tatu jioni.

1 Samweli 20:6 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Baba yako akinikosa kabisa, ndipo utasema, 'Daudi aliniomba kwa msisitizo ruhusa aondoke kwenda mjini kwake Bethlehemu; kwa sababu huko ni kipindi cha utoaji wa dhabihu ya mwaka kwa familia yao yote.'

1 Samweli 20:7 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kama atasema kuwa ni vyema, 'basi mtumishi wako atakuwa na amani. Lakini kama atakasirika sana, ndipo utajua kwamba ameamua kunitendea uovu.

1 Samweli 20:8 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa hiyo, umtendee wema mtumishi wako. Kwa maana umemweka mtumishi katika agano la BWANA pamoja na wewe. Lakini kama kuna dhambi ndani yangu, wewe mwenyewe uniuwe; maana kwa nini basi unipeleke kwa baba yako?”

1 Samweli 20:9 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yonathani akasema, “La hasha! Ikiwa ninajua kwamba baba ameamua baya likupate, siwezi kukuambia?”

1 Samweli 20:10 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ndipo Daudi akamwambia Yonathani, “Ni nani ataniambia ikiwa imetokea, baba yako akakujibu kwa ukali?”

1 Samweli 20:11 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yonathani akamwambia Daudi, “Njoo, hebu twende huko shambani.” Ndipo wote wakaondoka kwenda shambani.

1 Samweli 20:12 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yonathani akamwambia Daudi, “Na BWANA, Mungu wa Israeli, awe shahidi. Kesho muda kama huu, nitakuwa nimemuuliza baba yangu, au siku ya tatu, tazama, ikiwa kutakuwa na jambo zuri upande wa Daudi; je, nisikutumie taarifa na kulidhihirisha kwako?

1 Samweli 20:13 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Na kama ikimpendeza baba yangu akufanyie madhara, Basi BWANA ayafanye hayo kwa Yonathani na kuzidi ikiwa sitakujulisha jambo na kukupeleka mbali, ili kwamba uende kwa amani. Na BWANA awe pamoja nawe, kama alivyokuwa na baba yangu.

1 Samweli 20:14 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kama bado nikiwa hai, hautanionesha uaminifu wa agano la BWANA, kwamba siwezi kufa?

1 Samweli 20:15 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Na usivunje kabisa uaminifu wako wa agano kati yako na nyumba yangu, hata wakati BWANA atakapowaodoa kila mmoja wa adui za Daudi kutoka uso wa dunia.”

1 Samweli 20:16 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Basi Yonathani akafanya agano na nyumba ya Daudi na kusema, “Naye BWANA atawaondoa maadui wa Daudi.” (KISWAHILI IDIOM? ==== ULB ENGLISH IDIOM)

1 Samweli 20:17 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yonathani akamtaka Daudi aape tena kwa sababu ya upendo aliokuwa nao juu yake, kwa sababu alimpenda kama alivyopenda roho yake mwenyewe.

1 Samweli 20:18 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha Yonathani akamwambia Daudi, “Kesho ni siku ya mwezi mpya. Hautakuwapo, kwa sababu kiti chako kitakuwa wazi.

1 Samweli 20:19 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Utakapokuwa umekaa huko siku tatu, uende upesi hadi mahala ulipojificha mara ya kwanza, wakati shughuli ikifanyika, na ukaye karibu jiwe Ezeli.

1 Samweli 20:20 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Nitatupa mishale mitatu pembeni mwa jiwe, kama vile ninalenga kitu fulani.

1 Samweli 20:21 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha nitamtuma kijana wangu na kumwambia, 'Nenda utafute hiyo mishale.' Kama nitamwambia kijana hivi, 'Tazama, mishale iko upande huu wa kwako; kaichukue,” ndipo uje; maana hapo kutakuwa na usalama kwako na siyo madhara, kama BWANA aishivyo.

1 Samweli 20:22 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
“Lakini kama nikimwambia kijana hivi, 'Tazama, mishale iko mbele yako,' ndipo utakapokwenda zako, maana BWANA ametaka uende zako.

1 Samweli 20:23 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kulingana na makubaliano ambayo mimi na wewe tumeongea, angalia, BWANA yupo kati yangu na wewe milele.'”

1 Samweli 20:24 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa hiyo Daudi akajificha mle shambani. Pindi mwezi ulipoandama, mfalme aliketi chini ale chakula.

1 Samweli 20:25 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mfalme alikaa juu ya kiti chake, kama kawaida kwenye kiti karibu na ukuta. Yonathani alisimama wima, na Abneri alikaa ubavuni mwa Sauli. Lakini nafasi ya Daudi ilikuwa wazi.

1 Samweli 20:26 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hata hivyo Sauli hakusema kitu siku hiyo, kwa sababu alifikiri, “Kuna jambo limempata Daudi. Hayuko safi; hakika hayuko safi.”

1 Samweli 20:27 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini siku ya pili, siku moja baada ya mwandamo wa mwezi, bado nafasi ya Daudi ilikuwa tupu. Ndipo Sauli akamuuliza Yonathani mwanaye, “Kwa nini mwana wa Yese hakuja kwenye chakula, jana na hata leo?”

1 Samweli 20:28 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yonathani akamjibu Sauli, “Daudi aliomba kwangu ruhusa kwa dhati ili aende Bethlehemu.

1 Samweli 20:29 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Alisema, 'Tafadhali niruhusu niende. Maana familia yetu wanayo dhabihu huko mjini, na kaka yangu ameniagiza niwe huko. Basi kama nimepata kibali machoni pako, tafadhali niruhusu niende nikawaone kaka zangu.' Hakuja kwenye meza ya mfalme kwa sababu hii.”

1 Samweli 20:30 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ndipo hasira ya Sauli iliwaka juu ya Yonathani, na akamwambia, “Wee mwana wa mwanamke mkaidi na muasi! Wadhani kwamba sijui kuwa umemchagua Mwana wa Yese kwa ajili ya aibu yako, na kwa aibu ya uchi wa mama yako?

1 Samweli 20:31 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa kuwa mwana wa Yese anaishi duniani, siyo wewe wala ufalme wako utakaoimarika. Sasa basi, tuma watu wamlete kwangu, kwa sababu inampasa kufa.”

1 Samweli 20:32 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yonathani akamjibu Sauli baba yake, “Kwa sababu gani inampasa kuuwawa? Amefanya nini?”

1 Samweli 20:33 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ndipo Sauli akamtupia mkuki apate kumuua. Kwa hiyo Yonatani akatambua kwamba baba yake alinuia kumuua Daudi.

1 Samweli 20:34 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yonathani alitoka mezani akiwa na hasira kali bila kula chakula siku ya pili ya mwezi, kwa sababu alimhuzunikia Daudi, na kwa sababu baba yake amemwaibisha.

1 Samweli 20:35 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ikawa asubuhi, Yonathani akaenda huko shambani kama walivyoahidiana na Daudi, akiwa pamoja na kijana wake.

1 Samweli 20:36 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akamwambia yule kijana wake, “Kimbia utafute ile mishale niliyoitupa.” Na kijana alikimbia, akatupa mshale mwingine mbele yake.

1 Samweli 20:37 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kijana alipofika katika eneo ambapo mshale ulitua, ule alioutuma Yonathani, akamwita tena kijana, na kusema, “Huo mshale hauko mbele yako?”

1 Samweli 20:38 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha Yonathani akamwita yule kijana, “Upesi, harakisha, usikawie!” Hivyo kijana wa Yonathani akaikusanya mishale na kurudi kwa bwana wake.

1 Samweli 20:39 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini huyo kijana hakujua lolote. Ni Yonathani na Daudi tu ndio walijua habari yenyewe.

1 Samweli 20:40 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yonathani akampa kijana wake silaha na kumwambia, “Nenda, uzipeleke mjini.”

1 Samweli 20:41 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Punde tu kijana alipoondoka, Daudi akasimama kutokea upande wa kusini, akiwa amelala kifudifudi, akainama mara tatu. Walibusiana wao kwa wao na wote wakalia kwa pamoja, Daudi akilia zaidi.

1 Samweli 20:42 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yonathani akamwambia Daudi, “Nenda kwa amani, kwa sababu wote tumeapa kwa jina la BWANA na tulisema, 'BWANA awe kati yangu na wewe, na awe kati ya uzao wangu na uzao wako, milele.'” Kisha Daudi alisimama na akaondoka, na Yonathani akarudi mjini.
Previous Chapter
« 1 Samweli 19 (SWHULB)

Available Bible Translations

American Standard Version
1 Samuel 20 (ASV) »
King James Version
1 Samuel 20 (KJV) »
GOD’S WORD® (GW)
1 Samuel 20 (GW) »
World English Bible
1 Samuel 20 (WEB) »
Louis Segond 1910
1 Samuel 20 (LSG) »
इंडियन रिवाइज्ड वर्जन - हिंदी
1 शमूएल 20 (HINIRV) »
ਭਾਰਤੀ ਸੋਧਿਆ ਹੋਇਆ ਸੰਸਕਰਣ - ਪੰਜਾਬੀ
1 ਸਮੂਏਲ 20 (PANIRV) »
ভারতীয় সংশোধিত সংস্করণ - বাংলা
1 চমূৱেল 20 (BENIRV) »
இந்தியன் ரீவைஸ்டு வேர்ஷன் - தமிழ்
1 சாமுவேல் 20 (TAMIRV) »
इंडियन रिवाइज्ड वर्जन - मराठी
1 शमुवेल 20 (MARIRV) »
ఇండియన్ రేవిజ్డ్ వెర్షన్ - తెలుగు
1 సమూయేలు 20 (TELIRV) »
ઇન્ડિયન રિવાયઝ્ડ વર્ઝન - ગુજરાતી
1 શમુએલ 20 (GUJIRV) »
ಭಾರತೀಯ ಪರಿಷ್ಕೃತ ಆವೃತ್ತಿ - ಕನ್ನಡ
1 ಸಮುವೇಲನು 20 (KANIRV) »
الكتاب المقدس باللغة العربية، فان دايك
صَمُوئِيلَ ٱلْأَوَّلُ 20 (AVD) »
תנ ך עברי מודרני
שמואל א 20 (HEB) »
Bíblia Sagrada Português
1 Samuel 20 (BSL) »
Kinh Thánh: Tiếng Việt
1 Sa-mu-ên 20 (VIE) »
Reina Valera Antigua
1 Samuel 20 (RVA) »
La Sacra Bibbia
1 Samuele 20 (RIV) »
圣 经 简体中文和合本
撒 母 耳 记 上 20 (CUVS) »
聖 經 繁體中文和合本
撒 母 耳 記 上 20 (CUVT) »
Bibla e Shenjtë
1 Samuelit 20 (ALB) »
Библия на русском
1 Царств 20 (RUSV) »
Українська Біблія
1 Самуїлова 20 (UKR) »
Szent Biblia - Magyar
1 Sámuel 20 (KAR) »
Българска Библия
1 Царе 20 (BULG) »
Kitaabka Quduuska Ah
Samuu'eel Kowaad 20 (SOM) »
De Heilige Schrift
1 Samuël 20 (NLD) »
Dansk Bibel 1871
1 Samuel 20 (DA1871) »

1 Samweli (SWHULB) Chapter Selection

SWHULB Book Selection List