1 Samweli Chapter 25 SWHULB Bible Verse Images

1 Samweli 25 Bible Verse Pictures. Choose from a large collection of inspirational, motivational and encouraging Bible verses with pictures of nature. Download and share 1 Samweli 25 inspirational Bible verse images. Bible verse pictures were created based on verses from the Swahili Unlocked Literal Bible (SWHULB). The Holy Bible in the Swahili language, Unlocked Literal Bible version.

Copyright © 2019 Door43 World Missions Community
Language: Kiswahili (Swahili)
Translation by: Door43 World Missions Community

Contributors: Alfred Danjuma, Bariki Malisa, Christina Abraham Kileo, Cloud Roman, Daniel Marura Chacha, Dina Mast, Dina Roman, Donald Shadarck Dutuyi, Emmanuel Masanja Mbaaga, Emmanuel Nyamalya, Erasmus Peter Malelo, Ev. Lazaro Chalomhola, Ezekiel Manala, Fred, Gabriel Gidale Merus, Gabriel Lwitakubi Mazige, James Makula, James Semnkai, Jeremiah Masasi, Jesse Katabi Masolwa, John Ojasi, Joyce Gilbert Masasi, Karen Riecks, Kazwanomo, Kennedy, Ker, Lameck Yakobo Tobotobo, Laurent Petro Malelo, Lazarus David Chalomhola, Makene Mafwele, Marco Luma Mahushi, Mathew Nkusa, Mathias William, Mr. James Semnkai .It., Musa Isaya Majama, Musa Luzali, Pastor John Kerim, Pastor Jordan, Philipo Mussa Kanwelle, Raphael Musa, Rev. Charles Mabisa, Rev. Yohana Batano, Robert Ndalahwa, Sadiki Kulwa, Samson Nungwana, Thobias Kazwanomo, Yohana Dutuyi, Yohana Magera, Zelote Loilang'akaki Lukumay, Rev. Erasmus Peter Malelo, Ev. Mathew Kazimoto, Rev. Dr. David Magoke, Rev. Elias Ndema, Rev. Alex Nyuri, Rev. Gungutu Elias, Rev. Lameck Tobotobo, Rev. Catherin D. Matia, Rev. Yohana S Dutuyi, Rev. Donald Dutuyi, GS. Andrew Gewe, Ev. Ezekiel Daudi, Rev. John Ndaluka, Ev. Moses Malugu, Rev. Moses Eliakim Ndege, Past. Isack A. Gomugo, Past. Mathias William, Rev. Yekonia M. Koko, Rev. Elisande Mhanga, Ev. James A. Makula.

This translation is made available to you under the terms of the Creative Commons Attribution Share-Alike license 4.0.

You have permission to share and redistribute this Bible translation in any format and to make reasonable revisions and adaptations of this translation, provided that:

  • You include the above copyright and source information.
  • If you make any changes to the text, you must indicate that you did so in a way that makes it clear that the original licensor is not necessarily endorsing your changes.
  • If you redistribute this text, you must distribute your contributions under the same license as the original.

Credits: In addition, we would like to give very special thanks to eBible.org for making Swahili Unlocked Literal Bible available in MySQL format.


1 Samweli 25:1 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Basi Samweli akafariki. Waisraeli wote wakakusanyika pamoja na kumwomboleza, na wakamzika nyumbani kwake huko Rama. Kisha Daudi akainuka na akashuka hadi jangwa la Parani.

1 Samweli 25:2 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kulikuwa na mtu mmoja huko Maoni, na mali zake zilikuwa huko Karmali. Mtu huyo alikuwa tajiri sana. Alikuwa na kondoo elfu tatu na mbuzi elfu moja. Naye alikuwa akiwakata manyoya kondoo wake huko Karmeli.

1 Samweli 25:3 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Na mtu huyo aliitwa Nabali, na jina la mke wake aliitwa Abigaili. Mwanamke huyo alikuwa mwenye busara na mzuri kwa sura. Lakini mwanaume alikwa mkaidi na mwovu katika mambo yake. Alikuwa wa uzao wa nyumba ya Kalebu.

1 Samweli 25:4 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Daudi akasikia akiwa jangwani kwamba Nabali alikuwa akiwakata manyoya kondoo wake.

1 Samweli 25:5 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hivyo Daudi aliwatuma kwake vijana kumi. Akawaambia wale vijana, “Pandeni kwanda Karmeli, mwendeeni Nabali, na mkamsalimie kwa jina langu.

1 Samweli 25:6 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mtamwambia, 'Uishi katika baraka, Uwe na amani na nyumba yako iwe na amani, na wote ulionao wawe na amani.

1 Samweli 25:7 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Nasikia kwamba unao wakata manyoya. Wachungaji wako walikuwa pamoja nasi, na hatukuwafanyia ubaya, na muda wote wakiwa Karmeli hawakupotelewa kitu chochote.

1 Samweli 25:8 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Waulize vijana wako, nao watakuambia. Basi vijana wangu wapate kibali machoni pako, maana tumefika siku ya sherehe. Tafadhali utoe cho chote ulicho nacho mkononi kwa watumishi wako na kwa Daudi mwanao.'”

1 Samweli 25:9 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Vijana wa Daudi walipofika, walimwambia Nabali yote haya kwa niaba ya Daudi na kisha wakasubiri.

1 Samweli 25:10 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Nabali akawajibu watumishi wa Daudi, “Daudi ni nani? Na ni nani mwana wa Yese? Siku hizi wapo watumishi wengi wanaotoroka bwana zao.

1 Samweli 25:11 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Je, nichukue mkate wangu na maji yangu na nyama yangu ambayo nimewachinjia wakata manyoya wangu, na niwape watu wanaotoka nisikokujua?”

1 Samweli 25:12 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hivyo vijana wa Daudi waligeuka na kurudi, nakumwambia kila kitu kilichosemwa.

1 Samweli 25:13 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Daudi akawaambia watu wake, “Kila mtu ajifunge upanga wake.” Kila mtu akajifunga upanga wake. Daudi naye pia akajifunga upanga wake. Yapata kama watu mia nne wakafuatana na Daudi, na wengine mia mbili walibaki kulinda mizigo yao.

1 Samweli 25:14 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini kijana mmojawapo alimwambia Abigaili, mke wa Nabali akasema, “Daudi aliwatuma wajumbe kutoka jangwani waje wamsalimu bwana wetu, na yeye akawatukana.

1 Samweli 25:15 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Bado watu hawa walitutendea mema. Hatukudhurika na hatukupoteza chochote wakati wote tulipotembea nao tulipokuwa mbugani.

1 Samweli 25:16 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Walikuwa ukuta wetu usiku na mchana, wakati wote tulikuwa pamoja nao tukichunga kondoo.

1 Samweli 25:17 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa hiyo tambua hili na zingatia utafanya nini, maana ubaya unamvizia bwana wetu, na utakuwa juu ya nyumba yake yote. Yeye ni mtu asiyefaa na hakuna awezaye kushauriana naye.”

1 Samweli 25:18 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ndipo Abigaili akaharakisha na akachukuwa mikate mia mbili, chupa mbili za divai, kondoo watano waliokwisha andaliwa, vipimo vitano vya bisi, vishada mia moja vya zabibu, na mikate mia mbili ya tini na akavipakia juu ya punda.

1 Samweli 25:19 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akamwambia kijana wake, “Tangulia mbele yangu, nami nitakuja nyuma yako.” Lakini hakumwambia mmewe Nabali.

1 Samweli 25:20 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Alipokuwa akienda juu ya punda wake na kutelemka penye kificho cha mlima, Daudi na watu wake walishuka chini wakimwelekea Abigaili, naye akakutana nao.

1 Samweli 25:21 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Basi Daudi alikuwa amesema, “Hakika nimelinda bure vyote alivyonavyo mtu huyu huko nyikani, na vyote alivyonavyo hakuna kilichopotea, pamoja na hayo amenilipa mabaya badala ya mema.

1 Samweli 25:22 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mungu na anitendee hivyo mimi, Daudi, pia iwe zaidi, iwapo nitamwacha hata mtu mmoja wa kwake akiwa hai ifikapo kesho asubuhi.

1 Samweli 25:23 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Abigaili alipomwona Daudi, aliharakisha na kushuka chini ya punda wake, akalala kifudifudi na kujiinamisha hadi chini.

1 Samweli 25:24 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akamwangukia miguuni pake na kusema, “Juu yangu tu, bwana wangu, na uwe uovu. Tafadhali acha mjakazi wako aseme nawe, tena uyasikilize maneno ya mjakazi wako.

1 Samweli 25:25 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Nakusihi bwana wangu usimjali mtu huyu asiyefaa, Nabali, kwa maana kama jina lake lilivyo, ndivyo alivyo. Jina lake ni Nabali, na upumbavu uko pamoja naye. Lakini mimi mjakazi wako sikuwaona vijana wa bwana wangu, uliowatuma.

1 Samweli 25:26 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Sasa basi, bwana wangu, kama BWANA aishivyo, na kama unavyoishi, kwa kuwa BWANA amekuondoa kutoka kumwaga damu, na kuacha kulipiza kisasi kwa mkono mwenyewe, basi adui zako, na wale ambao wanatafuta kumfanyia uovu bwana wangu, wawe kama Nabali

1 Samweli 25:27 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Na sasa zawadi hii ambayo mjakazi wako ameileta kwa bwana wangu, na wapewe vijana ambao wanamfuata bwana wangu.

1 Samweli 25:28 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Tafadhali ulisamehe kosa la mjakazi wako, maana BWANA hakika atamfanyia bwana wangu nyumba imara, kwa sababu bwana wangu anapigana vita vya BWANA; na uovu hautaonekana ndani yako maadamu unaishi.

1 Samweli 25:29 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Na ingawa watu wangeinuka na kukuandama ili wakuue, bado uhai wa bwana wangu utafungwa katika furushi la walio hai na BWANA Mungu wako; na atayatupa maisha ya adui zako mbali, kama vile kutoka katika mfuko wa kombeo.

1 Samweli 25:30 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Na itakuwa, BWANA atakapokuwa amemtimizia bwana wangu mambo yote mazuri ambayo amekuahidi, na alivyokufanya kiongozi juu ya Israeli,

1 Samweli 25:31 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
jambo hili halitakuwa huzuni kwako, wala chukizo moyoni kwa bwana wangu, kwa sababu hukumwaga damu bila sababu, na hujajilipizia kisasi. Na BWANA akikuletea mafanikio, umkumbuke mjakazi wako.”

1 Samweli 25:32 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ndipo Daudi akamwambia Abigaili, “BWANA, Mungu wa Israeli, abarikiwe, aliyekutuma uonane na mimi leo.

1 Samweli 25:33 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Na hekima yako ibarikiwe, nawe umebarikiwa, kwa sababu leo umenizuia nisiwe na hatia ya kumwaga damu, na kutojilipizia kisasi kwa mkono wangu mwenyewe.

1 Samweli 25:34 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa kweli, kama BWANA, Mungu wa Israeli, aishivyo, ambaye amenizuia nisikuumize, kama usinge harakisha kuja ukutane nami, kwa hakika kesho asubuhi asinge salia hata mtoto mmoja wa kiume kwa Nabali.”

1 Samweli 25:35 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa hiyo Daudi akavipokea kutoka mkononi mwake vile alivyokuwa amemletea; akamwambia, “Nenda kwa amani hadi nyumbani kwako; tazama, nimeisikiliza sauti yako na nimekubali.”

1 Samweli 25:36 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Abigaili akarudi kwa Nabali; tazama, alikuwa akifanya sherehe katika mji wake, kama sherehe ya mfalme; na moyo wa Nabali ulifurahi ndani yake, kwa sababu alikwa amelewa sana. Kwa hiyo hakumwambia chochote kabisa hadi kulipopambazuka

1 Samweli 25:37 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ikawa asubuhi, divai ilipokuwa imemtoka Nabali, basi mkewe akamwambia mambo hayo; moyo wake ukafa ndani yake, na akawa kama jiwe.

1 Samweli 25:38 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ikawa baada ya siku kumi BWANA alimpiga Nabali naye akafa.

1 Samweli 25:39 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Naye Daudi aliposikia kwamba Nabali amekufa, akasema, “BWANA abarikiwe, aliyenichukulia hatua ya shutuma yangu kutoka mkono wa Nabali, na kumzuia mtumishi wake asifanye maovu. Na amemrudishia Nabali tendo la uovu juu ya kichwa chake mwenyewe.” Ndipo Daudi akawatuma watu wakaongee na Abigaili, ili amchukue awe mke wake.

1 Samweli 25:40 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Watumishi wake Daudi walipofika kwa Abigaili huko Karmeli, wakaongea naye na kusema, “Daudi ametutuma kwako tukuchukue hadi kwake uwe mke wake.”

1 Samweli 25:41 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Abigaili aliinuka, akainamisha uso chini, na akasema, “Tazama, mjakazi wako ni mtumwa aoshaye miguu ya watumishi wa bwana wangu.”

1 Samweli 25:42 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akaharakisha na kuamka, akapanda punda akiwa na vijakazi wake watano waliofuatana naye; akawafuata wajumbe wa Daudi, na akawa mke wake.

1 Samweli 25:43 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Daudi pia alimchukua Ahinoamu wa Yezreeli akamwoa; wote wawili wakawa wake zake.

1 Samweli 25:44 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakati huo Sauli alikuwa amempa Palti, mwana wa Laishi mtu wa Galimu, Mikali, binti yake, aliyekuwa mke wa Daudi.
Previous Chapter
« 1 Samweli 24 (SWHULB)

Available Bible Translations

American Standard Version
1 Samuel 25 (ASV) »
King James Version
1 Samuel 25 (KJV) »
GOD’S WORD® (GW)
1 Samuel 25 (GW) »
World English Bible
1 Samuel 25 (WEB) »
Louis Segond 1910
1 Samuel 25 (LSG) »
इंडियन रिवाइज्ड वर्जन - हिंदी
1 शमूएल 25 (HINIRV) »
ਭਾਰਤੀ ਸੋਧਿਆ ਹੋਇਆ ਸੰਸਕਰਣ - ਪੰਜਾਬੀ
1 ਸਮੂਏਲ 25 (PANIRV) »
ভারতীয় সংশোধিত সংস্করণ - বাংলা
1 চমূৱেল 25 (BENIRV) »
இந்தியன் ரீவைஸ்டு வேர்ஷன் - தமிழ்
1 சாமுவேல் 25 (TAMIRV) »
इंडियन रिवाइज्ड वर्जन - मराठी
1 शमुवेल 25 (MARIRV) »
ఇండియన్ రేవిజ్డ్ వెర్షన్ - తెలుగు
1 సమూయేలు 25 (TELIRV) »
ઇન્ડિયન રિવાયઝ્ડ વર્ઝન - ગુજરાતી
1 શમુએલ 25 (GUJIRV) »
ಭಾರತೀಯ ಪರಿಷ್ಕೃತ ಆವೃತ್ತಿ - ಕನ್ನಡ
1 ಸಮುವೇಲನು 25 (KANIRV) »
الكتاب المقدس باللغة العربية، فان دايك
صَمُوئِيلَ ٱلْأَوَّلُ 25 (AVD) »
תנ ך עברי מודרני
שמואל א 25 (HEB) »
Bíblia Sagrada Português
1 Samuel 25 (BSL) »
Kinh Thánh: Tiếng Việt
1 Sa-mu-ên 25 (VIE) »
Reina Valera Antigua
1 Samuel 25 (RVA) »
La Sacra Bibbia
1 Samuele 25 (RIV) »
圣 经 简体中文和合本
撒 母 耳 记 上 25 (CUVS) »
聖 經 繁體中文和合本
撒 母 耳 記 上 25 (CUVT) »
Bibla e Shenjtë
1 Samuelit 25 (ALB) »
Библия на русском
1 Царств 25 (RUSV) »
Українська Біблія
1 Самуїлова 25 (UKR) »
Szent Biblia - Magyar
1 Sámuel 25 (KAR) »
Българска Библия
1 Царе 25 (BULG) »
Kitaabka Quduuska Ah
Samuu'eel Kowaad 25 (SOM) »
De Heilige Schrift
1 Samuël 25 (NLD) »
Dansk Bibel 1871
1 Samuel 25 (DA1871) »

1 Samweli (SWHULB) Chapter Selection

SWHULB Book Selection List