Yeremia Chapter 32 SWHULB Bible Verse Images

Yeremia 32 Bible Verse Pictures. Choose from a large collection of inspirational, motivational and encouraging Bible verses with pictures of nature. Download and share Yeremia 32 inspirational Bible verse images. Bible verse pictures were created based on verses from the Swahili Unlocked Literal Bible (SWHULB). The Holy Bible in the Swahili language, Unlocked Literal Bible version.

Copyright © 2019 Door43 World Missions Community
Language: Kiswahili (Swahili)
Translation by: Door43 World Missions Community

Contributors: Alfred Danjuma, Bariki Malisa, Christina Abraham Kileo, Cloud Roman, Daniel Marura Chacha, Dina Mast, Dina Roman, Donald Shadarck Dutuyi, Emmanuel Masanja Mbaaga, Emmanuel Nyamalya, Erasmus Peter Malelo, Ev. Lazaro Chalomhola, Ezekiel Manala, Fred, Gabriel Gidale Merus, Gabriel Lwitakubi Mazige, James Makula, James Semnkai, Jeremiah Masasi, Jesse Katabi Masolwa, John Ojasi, Joyce Gilbert Masasi, Karen Riecks, Kazwanomo, Kennedy, Ker, Lameck Yakobo Tobotobo, Laurent Petro Malelo, Lazarus David Chalomhola, Makene Mafwele, Marco Luma Mahushi, Mathew Nkusa, Mathias William, Mr. James Semnkai .It., Musa Isaya Majama, Musa Luzali, Pastor John Kerim, Pastor Jordan, Philipo Mussa Kanwelle, Raphael Musa, Rev. Charles Mabisa, Rev. Yohana Batano, Robert Ndalahwa, Sadiki Kulwa, Samson Nungwana, Thobias Kazwanomo, Yohana Dutuyi, Yohana Magera, Zelote Loilang'akaki Lukumay, Rev. Erasmus Peter Malelo, Ev. Mathew Kazimoto, Rev. Dr. David Magoke, Rev. Elias Ndema, Rev. Alex Nyuri, Rev. Gungutu Elias, Rev. Lameck Tobotobo, Rev. Catherin D. Matia, Rev. Yohana S Dutuyi, Rev. Donald Dutuyi, GS. Andrew Gewe, Ev. Ezekiel Daudi, Rev. John Ndaluka, Ev. Moses Malugu, Rev. Moses Eliakim Ndege, Past. Isack A. Gomugo, Past. Mathias William, Rev. Yekonia M. Koko, Rev. Elisande Mhanga, Ev. James A. Makula.

This translation is made available to you under the terms of the Creative Commons Attribution Share-Alike license 4.0.

You have permission to share and redistribute this Bible translation in any format and to make reasonable revisions and adaptations of this translation, provided that:

  • You include the above copyright and source information.
  • If you make any changes to the text, you must indicate that you did so in a way that makes it clear that the original licensor is not necessarily endorsing your changes.
  • If you redistribute this text, you must distribute your contributions under the same license as the original.

Credits: In addition, we would like to give very special thanks to eBible.org for making Swahili Unlocked Literal Bible available in MySQL format.


Yeremia 32:1 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Neno likaja kwa Yeremia kutoka kwa Yahwe katika mwaka wa kumi wa Sedekia mfalme wa Yuda, katika mwaka wa kumi na nane wa Nebukadreza.

Yeremia 32:2 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Katika wakati huo, jeshsi la mfalme wa Babeli lilikuwa limeuzunguka Yerusalemu, na Nehemia nabii alikuwwa amefungwa katika uwanja wa walinzi katika nyumba ya mfalme wa Yuda.

Yeremia 32:3 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Sedekia mfalme wa Yuda alikuwa amemfunga na kusema, “Kwa nini unatabiri na kusema, 'Yahwe anasema hivi: Angalia, niko karibu kuweka mji huu katika mikono ya mfalme wa Babeli, na atauteka.

Yeremia 32:4 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Sedekia mfalme wa Yuda hatapona kutoka kwenye mikono ya Wakaldayo, kwa maana hakika atatiwa katika mkono wa mfalme wa Babeli. Mdomo wake utazumzia kwenye mdomo wa mfalme, na macho yake yatayaona macho ya mfalme.

Yeremia 32:5 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Atampeleka Sedekia Babeli, na atabaki huko hadi nimuadhibu—hili ni tangazo la Yahwe. Ingawa unapigana dhidi ya Wakaldayo, hautafanikiwa.”

Yeremia 32:6 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yeremia akasema, “Neno la Yahwe likaja kwangu, likisema, Angalia, Hanameli mwana wa Shalumu mjomba wako anakuja kwako na atasema,

Yeremia 32:7 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
“Linunue shamba langu ambalo liko katika Anathothi kwa ajili yako, kwa maana haki ya kununua ni yako.””

Yeremia 32:8 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha, kama Yahwe alivyotangaza, Hanameli, mwana wa mjomba wangu, akaja kwangu katika uwanja wa walinzi, na akasema kwangu, 'Linunue shamba langu kwa ajili yako ambalo liko Anathothi katika nchi ya Benyamini, kwa maana haki ya urithi ni ya kwako, na haki ya kulinunua ni yako. Linunue kwa ajili yako.' Kisha nilijua kuwa hili lilikuwa neno la Yahwe.

Yeremia 32:9 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa hiyo nililinua shamba katika Anathothi kutoka kwa Hanameli, mwana wa mjomba wangu, na nilipima fedha kwa ajili yake, shekeli kumi na saba katika uzito.

Yeremia 32:10 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha niliandika katika barua na kuitia muhuri, na kulikuwa na mashadi wakaishuhudia. Kisha nikampa fedha katika mizani.

Yeremia 32:11 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha nikaichukua hati ya manunuzi ambayo ilikuwa imepigwa muhuri, kwa kuifuata amri na taratibu, na kama ilivyo ada.

Yeremia 32:12 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ile barua nikampa Baruku mwana wa Neria wa Maaseya mbele ya Hanameli, mwana wa mjomba wangu, na mashahidi waliotia sahihi kwenye barua iliyopigwa muhuri, na mbele ya Wayahudi wote waliokaa katika uwanja wa walinzi.

Yeremia 32:13 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa hiyo nikampa amri Baruku mbele yao. Nilisema,

Yeremia 32:14 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yahwe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Chukua nyaraka hizi, vyote hati hii ya manunuzi iliyopigwa muhuri na nakala zisizopigwa muhuri za manunuzi, na uziweke katika chungu cha udongo ili vidumu kwa muda mrefu.

Yeremia 32:15 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa maana Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Nyumba, mashamba, na mashamba ya mizabibu vitanunuliwa tena katika nchi hii.

Yeremia 32:16 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Baada ya kumpa Baruki mwana wa Neria ile hati ya manunuzi, nikaomba kwa Yahwe nikasema,

Yeremia 32:17 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ole, Bwana Yahwe! Angalia! Wewe peke yako umezitengeneza mbingu na dunia kwa nguvu zako kuu na kwa mkono wako ulioinuka. Hakuna kitu ambacho ukisema kwako ni kigumu sana kukifanya.

Yeremia 32:18 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wewe huonesha agano la uaminifu kwa maelfu na kumimina makosa ya wanadamu katika mapaja ya watoto wao baada yao. Wewe ni Mungu mkuu na mwenye nguvu.

Yeremia 32:19 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wewe ni mkuu katika hekima na una nguvu katika matendo, kwa maana macho yako yanaona njia zote za watu, ili kumlipa kila mtu stahiki ya matendo yake.

Yeremia 32:20 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ulifanya ishara na maajabu katika nchi ya Misiri. Hata leo hapa Israeli na kati ya wanadamu wengine wote, umelifanya jina lako kuwa maarufu.

Yeremia 32:21 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa maana uliwanunua watu wako Israeli kwa ishira na maajabu, kwa mkono hodari, kwa mkono ulioinuka, na kwa hofu kuu.

Yeremia 32:22 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha uliwapa nchi hii—ambayo uliapa kwa babu zao kwamba utawapa—nchi itiririkayo maziwa na asali.

Yeremia 32:23 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hivyo walingia na kuimiliki. Lakini hawakuitii sauti yako wala kuishi kwa kuitii sheria yako. Hawakufanya chochote ulichowaamuru kufanya, kwa hiyo umeleta juu yao majanga haya yote.

Yeremia 32:24 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Angalia! Urefu wa maboma haya umefika hadi kwenye mji ili kuuteka. Kwa sababu ya upanga, njaa, na tauni, mji umetiwa kwenye mikono ya Wakaldayo wanaopigana dhidi yake. Kwa maana ulichosema kitatokea sasa kinatokea, na ona, unatazama.

Yeremia 32:25 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha wewe mwenyewe uliniambia, “Nunua shamba kwa fedha kwa ajili yako na mashahidi wameshuhudia, ingawa mji huu unatiwa mikononi mwa Wakaldayo.””

Yeremia 32:26 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Neno la Mungu likaja kwa Yeremia, likisema,

Yeremia 32:27 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
“Angalia! Mimi ni Yahwe, Mungu wa wanadamu wote. Kuna kitu cho chote kigumu sana kwangu kukifanya?

Yeremia 32:28 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa hiyo Yahwe anasema hivi, 'Ona, niko karibu kuutia mji huu kwenye mikono ya Wakaldayo na Nebukadreza, mfalme wa Babeli. Atauteka.

Yeremia 32:29 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakaldayo wanaopigana dhidi ya mji huu watakuja na kuwasha moto kwenye mji huu na kuunguza, pamoja na nyumba juu ya paa la watu waliomwabudu Baali na kumimina dhabihu kwa miungu wengine ili kunikasirisha.

Yeremia 32:30 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa maana watu wa Israeli na Yuda hakika wamekuwa watu wanaofanya maovu mbele ya macho yangu tangu ujana wao. Watu wa Israeli hakika wameniudhi kwa matendo ya mikono yao—hili ni tangazo la Yahwe.

Yeremia 32:31 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yahwe anatangaza kwamba mji huu umekuwa sababu ya hasira yangu na ghadhabu yangu tangu siku walipoujenga. Umekuwa hivyo hata leo. Kwa hiyo nitaundoa mbele ya uso wangu

Yeremia 32:32 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
kwa sababu ya uovu wote wa watu wa Israeli na Yuda, mambo waliyofanya ili kunichukiza—wao, wafalme wao, wana wa wafalme, makuhani, manabii, na kila mtu katika Yuda na wakaaji wa Yerusalemu.

Yeremia 32:33 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wamenigeuzia migongo yao badala ya nyuso zao, ingawa niliwafundisha kwa furaha. Nilijitahidi kuwafundisha, lakini hakuna hata mmoja wao aliyenisikiliza ili kupokea marekebisho.

Yeremia 32:34 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Walisimamisha sanamu zao za ajabu katika nyumba inayoitwa kwa jina langu, ili kunitia unajisi.

Yeremia 32:35 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakazijenga sehemu za juu katika Bonde la Beni Hinomu ili kuwatia katika moto wana wao na binti zao kwa ajili ya Moleki. Mimi sikuwaagiza. Sikuweka akilini mwangu kamwe kwamba watafanya mambo maovu na kwa hiyo kuwasabisha Yuda watende dhambi.

Yeremia 32:36 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa hiyo sasa, Mimi, Yahwe, Mungu wa Israeli, kuhusu mji huu ninasema hivi, 'mji ambao mnasema, 'Umetiwa mikononi mwa mfalme wa Babeli kwa upanga, njaa, na pigo.'

Yeremia 32:37 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ona, niko karibu kuwakusanya kutoka kila nchi nilikowapeleka katika hasira yangu, ghadhabu, hasira kuu. Niko karibu kuwarudisha kwenye sehemu hii na kuwawezesha kuishi katika usalama.

Yeremia 32:38 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao.

Yeremia 32:39 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Nitawapa moyo mmjoa na na njia moja ya kuniheshimu kila siku ili kwamba yawepo mema kwa ajili yao na uzao wao baada yao.

Yeremia 32:40 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha nitafanya pamoja nao agano la milele, ili nisiache kufanya mema kwa ajili yao. nitajiwekea heshima katika mioyo yao, ili kwamba wasiniache.

Yeremia 32:41 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha nitajifurahisha katika kufanya mema kwao. Kwa uaminifu nitawapanda katika anchi hii kwa moyo wangu wote na maisha yangu yoye.

Yeremia 32:42 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa amaana Yahwe anasema hivi, 'Kama tu nilivyoyaleta majanga haya makubwa yote juu ya watu hawa, hivyo hivyo nitaleta juu yao mambo mema niliyosema kwamba nitafanya kwa ajili yao.

Yeremia 32:43 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Basi mashamba yatanunuliwa katika nchi hii, ambayo mnaisema, “Hii ni nchi iliyoharibiwa, isiyo na mwanadamu wala mnyama. Imetiwa mikononi mwa Wakaldayo”

Yeremia 32:44 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Watanunua mashamba kwa fedha na kuandika katika barua zilizopigwa muhuri. Watawakusanya mashahidi katika nchi ya Benyamini, wote kuzunguka Yerusalemu na miji ya Yuda katika miji ya nchi yenye vilima, na katika nchi tambarare, na katika miji ya Negebu. Kwa maana nitawarejesha wafungwa wao—hili ni tangazo la Yahwe.”'
Previous Chapter
« Yeremia 31 (SWHULB)

Available Bible Translations

American Standard Version
Jeremiah 32 (ASV) »
King James Version
Jeremiah 32 (KJV) »
GOD’S WORD® (GW)
Jeremiah 32 (GW) »
World English Bible
Jeremiah 32 (WEB) »
Louis Segond 1910
Jérémie 32 (LSG) »
Luther Bibel 1912
Jeremia 32 (LUTH1912) »
इंडियन रिवाइज्ड वर्जन - हिंदी
यिर्मयाह 32 (HINIRV) »
ਭਾਰਤੀ ਸੋਧਿਆ ਹੋਇਆ ਸੰਸਕਰਣ - ਪੰਜਾਬੀ
ਯਿਰਮਿਯਾਹ 32 (PANIRV) »
ভারতীয় সংশোধিত সংস্করণ - বাংলা
যিৰিমিয়া 32 (BENIRV) »
இந்தியன் ரீவைஸ்டு வேர்ஷன் - தமிழ்
எரேமியா 32 (TAMIRV) »
इंडियन रिवाइज्ड वर्जन - मराठी
यिर्मया 32 (MARIRV) »
ఇండియన్ రేవిజ్డ్ వెర్షన్ - తెలుగు
యిర్మీయా 32 (TELIRV) »
ઇન્ડિયન રિવાયઝ્ડ વર્ઝન - ગુજરાતી
યર્મિયા 32 (GUJIRV) »
ಭಾರತೀಯ ಪರಿಷ್ಕೃತ ಆವೃತ್ತಿ - ಕನ್ನಡ
ಯೆರೆಮೀಯನು 32 (KANIRV) »
الكتاب المقدس باللغة العربية، فان دايك
إِرْمِيَا 32 (AVD) »
תנ ך עברי מודרני
ירמיה 32 (HEB) »
Bíblia Sagrada Português
Jeremias 32 (BSL) »
Kinh Thánh: Tiếng Việt
Giê-rê-mi-a 32 (VIE) »
Reina Valera Antigua
Jeremías 32 (RVA) »
La Sacra Bibbia
Geremia 32 (RIV) »
圣 经 简体中文和合本
耶 利 米 书 32 (CUVS) »
聖 經 繁體中文和合本
耶 利 米 書 32 (CUVT) »
Bibla e Shenjtë
Jeremia 32 (ALB) »
Svenska Bibeln 1917
Jeremia 32 (SV1917) »
Библия на русском
Иеремия 32 (RUSV) »
Українська Біблія
Єремія 32 (UKR) »
Szent Biblia - Magyar
Jeremiás 32 (KAR) »
Българска Библия
Еремия 32 (BULG) »
Det Norsk Bibel
Jeremia 32 (NORSK) »
Kitaabka Quduuska Ah
Yeremyaah 32 (SOM) »
De Heilige Schrift
Jeremia 32 (NLD) »
Dansk Bibel 1871
Jeremias 32 (DA1871) »

Yeremia (SWHULB) Chapter Selection

SWHULB Book Selection List