Waamuzi Chapter 11 SWHULB Bible Verse Images

Waamuzi 11 Bible Verse Pictures. Choose from a large collection of inspirational, motivational and encouraging Bible verses with pictures of nature. Download and share Waamuzi 11 inspirational Bible verse images. Bible verse pictures were created based on verses from the Swahili Unlocked Literal Bible (SWHULB). The Holy Bible in the Swahili language, Unlocked Literal Bible version.

Copyright © 2019 Door43 World Missions Community
Language: Kiswahili (Swahili)
Translation by: Door43 World Missions Community

Contributors: Alfred Danjuma, Bariki Malisa, Christina Abraham Kileo, Cloud Roman, Daniel Marura Chacha, Dina Mast, Dina Roman, Donald Shadarck Dutuyi, Emmanuel Masanja Mbaaga, Emmanuel Nyamalya, Erasmus Peter Malelo, Ev. Lazaro Chalomhola, Ezekiel Manala, Fred, Gabriel Gidale Merus, Gabriel Lwitakubi Mazige, James Makula, James Semnkai, Jeremiah Masasi, Jesse Katabi Masolwa, John Ojasi, Joyce Gilbert Masasi, Karen Riecks, Kazwanomo, Kennedy, Ker, Lameck Yakobo Tobotobo, Laurent Petro Malelo, Lazarus David Chalomhola, Makene Mafwele, Marco Luma Mahushi, Mathew Nkusa, Mathias William, Mr. James Semnkai .It., Musa Isaya Majama, Musa Luzali, Pastor John Kerim, Pastor Jordan, Philipo Mussa Kanwelle, Raphael Musa, Rev. Charles Mabisa, Rev. Yohana Batano, Robert Ndalahwa, Sadiki Kulwa, Samson Nungwana, Thobias Kazwanomo, Yohana Dutuyi, Yohana Magera, Zelote Loilang'akaki Lukumay, Rev. Erasmus Peter Malelo, Ev. Mathew Kazimoto, Rev. Dr. David Magoke, Rev. Elias Ndema, Rev. Alex Nyuri, Rev. Gungutu Elias, Rev. Lameck Tobotobo, Rev. Catherin D. Matia, Rev. Yohana S Dutuyi, Rev. Donald Dutuyi, GS. Andrew Gewe, Ev. Ezekiel Daudi, Rev. John Ndaluka, Ev. Moses Malugu, Rev. Moses Eliakim Ndege, Past. Isack A. Gomugo, Past. Mathias William, Rev. Yekonia M. Koko, Rev. Elisande Mhanga, Ev. James A. Makula.

This translation is made available to you under the terms of the Creative Commons Attribution Share-Alike license 4.0.

You have permission to share and redistribute this Bible translation in any format and to make reasonable revisions and adaptations of this translation, provided that:

  • You include the above copyright and source information.
  • If you make any changes to the text, you must indicate that you did so in a way that makes it clear that the original licensor is not necessarily endorsing your changes.
  • If you redistribute this text, you must distribute your contributions under the same license as the original.

Credits: In addition, we would like to give very special thanks to eBible.org for making Swahili Unlocked Literal Bible available in MySQL format.


Waamuzi 11:1 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yeftha Mgileadi alikuwa shujaa mwenye nguvu, lakini alikuwa mwana wa kahaba. Gileadi alikuwa baba yake.

Waamuzi 11:2 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mke wa Gileadi pia alizaa wanawe wengine. Wana wa mkewe walipokua, walimlazimisha Yeftha aondoke nyumbani na kumwambia, “Huwezi kurithi chochote kutoka katika familia yetu. Wewe ni mwana wa mwanamke mwingine.”

Waamuzi 11:3 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Basi Yeftha akaondoka toka kwa ndugu zake, akaishi katika nchi ya Tobu. Watu wasiokuwa na sheria waliungana na Yeftha na wakaja na kwenda pamoja naye.

Waamuzi 11:4 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Siku kadhaa baadaye, wana wa Amoni walipigana na Israeli.

Waamuzi 11:5 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wana wa Amoni walipopigana na Israeli, wazee wa Gileadi wakaenda kumleta Yeftha kutoka nchi ya Tobu.

Waamuzi 11:6 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakamwambia Yeftha, “Njoo uwe kiongozi wetu ili tupigane na wana wa Amoni.”

Waamuzi 11:7 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
YEphtha akawaambia viongozi wa Gileadi, “mlinichukia na kunilazimisha kuondoka nyumbani kwa baba yangu. Kwa nini mnakuja kwangu sasa munapokuwa na shida?”

Waamuzi 11:8 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wazee wa Gileadi wakamwambia Yeftha, “Ndiyo sababu tunakugeukia sasa; njoo pamoja nasi pigana na watu wa Amoni, na wewe utakuwa kiongozi juu ya wote wanaoishi Gileadi.

Waamuzi 11:9 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yeftha akawaambia wazee wa Gileadi, “Ikiwa mnanirejesha nyumbani tena ili kupigana na wana wa Amoni, na kama Bwana atatupa ushindi juu yao, nitakuwa kiongozi wenu.”

Waamuzi 11:10 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
wazee wa Gileadi wakamwambia Yeftha, “Bwana awe shahidi kati yetu ikiwa hatutafanya kama tunavyosema!”

Waamuzi 11:11 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yeftha akaenda pamoja na wazee wa Gileadi, nao watu wakamfanya awe msimamizi na mkuu juu yao. Alipokuwa mbele ya Bwana huko Mizpa, Yeftha akarudia ahadi zote alizozifanya.

Waamuzi 11:12 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ndipo Yeftha akatuma wajumbe kwa mfalme wa wana wa Amoni, akisema, “Ni nini mgogoro huu kati yetu? Kwa nini umekuja kwa nguvu kuchukua ardhi yetu?”

Waamuzi 11:13 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mfalme wa wana wa Amoni akawajibu wajumbe wa Yeftha, “Kwa sababu Israeli walipopanda kutoka Misri, walichukua nchi yangu toka Arnoni hata Yaboki, mpaka Yordani. Sasa rudisha ardhi hizo kwa amani.”

Waamuzi 11:14 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yefta akatuma tena wajumbe kwa mfalme wa wana wa Amoni,

Waamuzi 11:15 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
akasema, “Yefita asema hivi, Israeli hawakuchukua nchi ya Moabu na nchi ya wana wa Amoni;

Waamuzi 11:16 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
lakini walitoka Misri, na Israeli wakaenda kupitia jangwa hadi Bahari ya Shamu na Kadeshi.

Waamuzi 11:17 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Israeli walipomtuma wajumbe kwa mfalme wa Edomu, wakisema, 'Tafadhali tunaomba ruhusa tupite katika nchi yako,' mfalme wa Edomu hakuwasikiliza. Wakawatuma wajumbe kwa mfalme wa Moabu, lakini akakataa. Basi Israeli wakakaa Kadeshi.

Waamuzi 11:18 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha wakapitia jangwani, wakaondoka katika nchi ya Edomu, na nchi ya Moabu; wakavuka upande wa mashariki wa nchi ya Moabu, wakapanga ng'ambo ya Arnoni. Lakini hawakuingia mpaka wa Moabu, maana Arnoni ilikuwa mpaka wa Moabu.

Waamuzi 11:19 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Israeli wakatuma wajumbe kwa Sihoni, mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni; Israeli akamwambia, 'Tafadhali, tunaomba tupite katika nchi yako hata mahali petu.'

Waamuzi 11:20 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini Sihoni hakumwamini Israeli apite katika eneo lake. Basi Sihoni akakusanya jeshi lake lote, akalipeleka Yahasa, na huko akapigana na Israeli

Waamuzi 11:21 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Bwana, Mungu wa Israeli, akamtia Sihoni na watu wake wote mkononi mwa Israeli, nao wakawashinda. Basi Israeli wakachukua nchi yote ya Waamori waliokaa katika nchi hiyo.

Waamuzi 11:22 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wachukua kila kitu ndani ya wilaya ya Waamori, kutoka Arnoni hadi Yaboki, na kutoka jangwani hadi Yordani.

Waamuzi 11:23 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Basi, Bwana, Mungu wa Israeli, amewafukuza Waamori mbele ya watu wake Israeli, na sasa mnataka kuimiliki nchi yao?

Waamuzi 11:24 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Je, huwezi kuchukua nchi ambayo Kemoshi, mungu wako, anakupa? Kwa hiyo nchi yoyote Bwana, Mungu wetu, ametupa, tutachukua.

Waamuzi 11:25 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Sasa wewe ni bora zaidi kuliko Balaki, mwana wa Sipori, mfalme wa Moabu? Je, alidai kuwa na hoja na Israeli? Je, yeye amewahi kupigana vita dhidi yao?

Waamuzi 11:26 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakati Israeli walipoishia miaka mia tatu huko Heshboni na vijiji vyake, na Aroeri na vijiji vyake, na katika miji yote iliyo karibu na Arnoni, kwa nini hamkuwachukua tena wakati huo?

Waamuzi 11:27 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Sijawafanyia vibaya, lakini mnanifanyia vibaya kwa kunishambulia. Bwana, mwamuzi, ataamua leo kati ya wana wa Israeli na wana wa Amoni.

Waamuzi 11:28 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini mfalme wa wana wa Amoni akakataa onyo alilotumiwa na Yeftha.

Waamuzi 11:29 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Basi, Roho wa Bwana akamjia Yeftha, akapita Gileadi na Manase, akapitia Mizpa ya Gileadi, na kutoka Mispa ya Gileadi akapita kwa wana wa Amoni.

Waamuzi 11:30 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yeftha akaahidi kwa Bwana, akasema, “Ikiwa utanipa ushindi juu ya wana wa Amoni,

Waamuzi 11:31 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
chochote kinachotoka mlangoni mwa nyumba yangu kunijia mimi nitakaporudi kwa amani kutoka kwa wana wa Amoni kitakuwa cha Bwana; Nami nitatoa hiyo sadaka ya kuteketezwa.”

Waamuzi 11:32 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Basi Yeftha akapita kwa wana wa Amoni ili kupigana nao, naye Bwana akampa ushindi.

Waamuzi 11:33 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akawashinda na kusababisha mauaji makubwa kutoka Aroeri hadi miji ishirini na miwili-na Abeli ​​Keramimu. Basi wana wa Amoni waliwekwa chini ya uangalizi wa watu wa Israeli.

Waamuzi 11:34 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yeftha alifika nyumbani kwake huko Mizpa, na binti yake akatoka kumlaki na ngoma na kucheza. Alikuwa mtoto wake pekee, na badala yake hakuwa na mwana wa kiume wala binti.

Waamuzi 11:35 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mara tu alipopomwona, alirarua nguo zake akasema, 'Loo! Binti yangu! Umenivunja kwa huzuni, na umekuwa mtu anayenisababishia maumivu yangu! Kwa maana nimeapa kwa Bwana, wala siwezi kurudisha ahadi yangu.

Waamuzi 11:36 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akamwambia, “Baba yangu, umeweka ahadi kwa Bwana, unifanyie kila kitu ulichoahidi; kwa kuwa Bwana amekulipia kisasi juu ya adui zako, wana wa Amoni.”

Waamuzi 11:37 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akamwambia baba yake, “Hebu ahadi hii ihifadhiwe kwa ajili yangu. Niache kwa miezi miwili, nipate kuondoka na kwenda kwenye vilima na kuomboleza juu ya ubikira wangu, mimi na wenzangu.”

Waamuzi 11:38 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akasema, “Nenda.” Alimtuma kwa muda wa miezi miwili. Akamwondoa, yeye na wenzake, nao wakauomboleza ubikira wake katika milimani.

Waamuzi 11:39 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mwishoni mwa miezi miwili alirudi kwa baba yake, ambaye alifanya kulingana na ahadi ya aliyoifanya. Sasa alikuwa hajalala na mwanaume, na ikawa desturi katika Israeli

Waamuzi 11:40 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
kwamba binti za Israeli kila mwaka, kwa siku nne, waweze kurejea hadithi ya binti ya Yeftha Mgileadi.
Previous Chapter
« Waamuzi 10 (SWHULB)

Available Bible Translations

American Standard Version
Judges 11 (ASV) »
King James Version
Judges 11 (KJV) »
GOD’S WORD® (GW)
Judges 11 (GW) »
World English Bible
Judges 11 (WEB) »
Louis Segond 1910
Juges 11 (LSG) »
Luther Bibel 1912
Richter 11 (LUTH1912) »
इंडियन रिवाइज्ड वर्जन - हिंदी
न्यायियों 11 (HINIRV) »
ਭਾਰਤੀ ਸੋਧਿਆ ਹੋਇਆ ਸੰਸਕਰਣ - ਪੰਜਾਬੀ
ਕਜ਼ਾૃ 11 (PANIRV) »
ভারতীয় সংশোধিত সংস্করণ - বাংলা
বিচাৰকর্তাবিলাক 11 (BENIRV) »
இந்தியன் ரீவைஸ்டு வேர்ஷன் - தமிழ்
நியாயாதிபதிகள் 11 (TAMIRV) »
इंडियन रिवाइज्ड वर्जन - मराठी
शास्ते 11 (MARIRV) »
ఇండియన్ రేవిజ్డ్ వెర్షన్ - తెలుగు
న్యాయాధిపతులు 11 (TELIRV) »
ઇન્ડિયન રિવાયઝ્ડ વર્ઝન - ગુજરાતી
ન્યાયાધીશો 11 (GUJIRV) »
ಭಾರತೀಯ ಪರಿಷ್ಕೃತ ಆವೃತ್ತಿ - ಕನ್ನಡ
ನ್ಯಾಯಸ್ಥಾಪಕರು 11 (KANIRV) »
الكتاب المقدس باللغة العربية، فان دايك
اَلْقُضَاة 11 (AVD) »
תנ ך עברי מודרני
שפטים 11 (HEB) »
Bíblia Sagrada Português
Juízes 11 (BSL) »
Kinh Thánh: Tiếng Việt
Các Thủ Lãnh 11 (VIE) »
Reina Valera Antigua
Jueces 11 (RVA) »
La Sacra Bibbia
Giudici 11 (RIV) »
圣 经 简体中文和合本
士 师 记 11 (CUVS) »
聖 經 繁體中文和合本
士 師 記 11 (CUVT) »
Bibla e Shenjtë
Gjyqtarët 11 (ALB) »
Svenska Bibeln 1917
Domarboken 11 (SV1917) »
Библия на русском
Книга Судей 11 (RUSV) »
Українська Біблія
Книга Суддів 11 (UKR) »
Szent Biblia - Magyar
Bírák 11 (KAR) »
Българска Библия
Съдии 11 (BULG) »
聖書 日本語
士師記 11 (JPN) »
Kitaabka Quduuska Ah
Xaakinnada 11 (SOM) »
De Heilige Schrift
Richtere 11 (NLD) »
Dansk Bibel 1871
Dommer 11 (DA1871) »

Waamuzi (SWHULB) Chapter Selection

SWHULB Book Selection List