Hesabu Chapter 18 SWHULB Bible Verse Images

Hesabu 18 Bible Verse Pictures. Choose from a large collection of inspirational, motivational and encouraging Bible verses with pictures of nature. Download and share Hesabu 18 inspirational Bible verse images. Bible verse pictures were created based on verses from the Swahili Unlocked Literal Bible (SWHULB). The Holy Bible in the Swahili language, Unlocked Literal Bible version.

Copyright © 2019 Door43 World Missions Community
Language: Kiswahili (Swahili)
Translation by: Door43 World Missions Community

Contributors: Alfred Danjuma, Bariki Malisa, Christina Abraham Kileo, Cloud Roman, Daniel Marura Chacha, Dina Mast, Dina Roman, Donald Shadarck Dutuyi, Emmanuel Masanja Mbaaga, Emmanuel Nyamalya, Erasmus Peter Malelo, Ev. Lazaro Chalomhola, Ezekiel Manala, Fred, Gabriel Gidale Merus, Gabriel Lwitakubi Mazige, James Makula, James Semnkai, Jeremiah Masasi, Jesse Katabi Masolwa, John Ojasi, Joyce Gilbert Masasi, Karen Riecks, Kazwanomo, Kennedy, Ker, Lameck Yakobo Tobotobo, Laurent Petro Malelo, Lazarus David Chalomhola, Makene Mafwele, Marco Luma Mahushi, Mathew Nkusa, Mathias William, Mr. James Semnkai .It., Musa Isaya Majama, Musa Luzali, Pastor John Kerim, Pastor Jordan, Philipo Mussa Kanwelle, Raphael Musa, Rev. Charles Mabisa, Rev. Yohana Batano, Robert Ndalahwa, Sadiki Kulwa, Samson Nungwana, Thobias Kazwanomo, Yohana Dutuyi, Yohana Magera, Zelote Loilang'akaki Lukumay, Rev. Erasmus Peter Malelo, Ev. Mathew Kazimoto, Rev. Dr. David Magoke, Rev. Elias Ndema, Rev. Alex Nyuri, Rev. Gungutu Elias, Rev. Lameck Tobotobo, Rev. Catherin D. Matia, Rev. Yohana S Dutuyi, Rev. Donald Dutuyi, GS. Andrew Gewe, Ev. Ezekiel Daudi, Rev. John Ndaluka, Ev. Moses Malugu, Rev. Moses Eliakim Ndege, Past. Isack A. Gomugo, Past. Mathias William, Rev. Yekonia M. Koko, Rev. Elisande Mhanga, Ev. James A. Makula.

This translation is made available to you under the terms of the Creative Commons Attribution Share-Alike license 4.0.

You have permission to share and redistribute this Bible translation in any format and to make reasonable revisions and adaptations of this translation, provided that:

  • You include the above copyright and source information.
  • If you make any changes to the text, you must indicate that you did so in a way that makes it clear that the original licensor is not necessarily endorsing your changes.
  • If you redistribute this text, you must distribute your contributions under the same license as the original.

Credits: In addition, we would like to give very special thanks to eBible.org for making Swahili Unlocked Literal Bible available in MySQL format.


Hesabu 18:1 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
BWANA akamwambia Haruni, “Wewe, wana wako, na uzao wa baba yako watawajibika kwa dhambi zote zilizotendwa mahali patakatifu. Lakini wewe na wana wako pekee mtawajibika kwa uovu uliofanywa na yeyote mahali patakatifu.

Hesabu 18:2 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Na ndugu zako nao wa kabila ya Lawi, kabila la ukoo wako, utawaleta pamoja na wewe ili kwamba waweze kuungana na wewe ili wakusaidie wakati wewe na wanao mnapokuwa mnatumikia mbele ya hema ya amri ya agano.

Hesabu 18:3 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Watakutumikia wewe na hema yote. Hata hivyo, wasisogee karibu na chochote ndani ya mahali patakatifu au kitu chochote kilichounganishwa na madhabahu, vinginevyo wewe na wao mtakufa.

Hesabu 18:4 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wataungana na wewe na kuitunza hema ya kukutania, kwa kazi zote zinazohusiana na hema. Mtu mgeni asikusogelee.

Hesabu 18:5 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wewe utaajibika kwa ajili ya mahali patakatifu na kwa ajili ya madhabahu ili kwamba hasira yangu isiwajilie watu wa Israeli tena.

Hesabu 18:6 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Tazama, Mmi mwenyewe nimewachagua ndugu zako wa kabila ya Walawi kutoka mioingoni mwa uzao wa Israeli. Wao ni zawadi kwako. walitolewa kwangu ili waifanye kazi inayohusiana na hema ya kukutania.

Hesabu 18:7 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini ni wewe pekee yako na wanao ndio mnaoruhusiwa kufanya kazi ya ukuhani kuhusiana na kila kitu kilichounganishwa na madhabahu na kitu chochote ndani ya lile pazia. Wewe mwenyewe lazima ukamilishe majukumu hayo. Mimi ninakupa ukuhani kama zawadi. Mgeni yeyote anayekaribia atauawa.”

Hesabu 18:8 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha BWANA akamwambia Haruni, “Tazama, Nimekupa majukumu ya kusimamia sadaka za kuinuliwa kwangu, na sadaka zengine takatifu ambazo wana wa Israeli wanatoa kwangu. Nimekupa sadaka hizi wewe na wana wako kuwa haki yako milele.

Hesabu 18:9 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hivi ni vitu vitakatifu sana, amabavyo visiteketezwe kwa moto: kutoka kwenye sadaka zao-kila sadaka ya unga, kila sadaka ya dhambi, na kila sadaka ya hatia- ni vitu vitakatifu sana kwa ajili yako na wana wako.

Hesabu 18:10 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Sadaka hizi ni takatifu sana; kila mume lazima aile, kwa kuwa ni vitakatifu kwako.

Hesabu 18:11 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hizi ni sadaka ambazo zitakuwa zako: Sadaka zao, sadaka zote za kuinuliwa za wana wa Israeli. Nimekupa wewe, wana wako na binti zako kuwa gawio lako la milele. Kila mmoja ambaye ni msafi katika familia yako anaweza kula sadaka zozote katika hizi.

Hesabu 18:12 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mafuta yote mazuri, ile divai nzuri yote mpya na unga, malimbuko ambyo watu hutoa kwangu- vitu hivi vyote nimekupa wewe.

Hesabu 18:13 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mavuno ya kwanza yaliyoiva yaliyo katika ardhi yao ambayo wanaleta kwangu, yatakuwa yako. Kila mtu aliye msafi kwenye famila yako anaweza kula vitu hivi.

Hesabu 18:14 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kila kitu kilichotolewa wakfu katika Israeli kitakuwa chako.

Hesabu 18:15 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kila kitu kinachofungua tumbo, kila limbuko ambalo watu hutoa kwa BWANA, vyote vya watu na wanyama, vitakuwa vyako. Hata hivyo, watu lazima wawakomboe wazaliwa wa kwanza wa kiume, na watawakomboa wazaliwa wa kwanza wa wanyama wasio safi.

Hesabu 18:16 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wale ambao wanahitaji kukombolewa na watu watakombolewa wakiwa na umri wa mwezi mmoja. Ndipo watu watawakomboa kwa bei ya shekeli tano, kwa kiwango cha shekeli za mahali patakatifu, ambacho ni sawa na gera ishirini.

Hesabu 18:17 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini mzaliwa wa kwanza wa ng'ombe, au mzaliwa wa kwana wa kondoo, au mzaliwa wa kwanza wa mbuzi-msiwakomboe hawa wanyama, wametengwa kwa ajili yangu. Utanyunyizia damu yake madhabahuni na kuteketeza mafuta yao kama sadaka ya moto, ambayo ni harufu nzuri ya kumpendeza BWANA.

Hesabu 18:18 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Nyama yao itakuwa yako. Kama kidali cha kuinuliwa na paja la kulia, nyama yao itakuwa yako.

Hesabu 18:19 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Sadaka yote takatifu ambayo watu wa Israeli wanaitoa kwa BWANA, nimekupa wewe, na wana wako na binti zako walio pamoja nawe. Kama gawio la kudumu. Hili ni agano la milele la chumvi, agano linalofunga milele, mbele za BWANA kwako wewe na uzao wako walio pamoja na wewe.”

Hesabu 18:20 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
BWANA akasema na Haruni. “hautakuwa na urithi katika ardhi ya watu, wala hautakuwa na gawio miongoni mwa watu. Mimi ndimi gawiio lenu na urithi wenu miongoni mwa watu wa Israeli.

Hesabu 18:21 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Tazama, Nimewapatia uzao wa Lawi, zaka zote za Israeli kuwa urithi wao kwa sababu ya huduma wanayotoa katika hema ya kukutania.

Hesabu 18:22 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kuanzi a sasa, watu wa Israeli wasisogee karibu na hema ya kukutania, vinginevyo wataajibika kwa dhambi hii na kufa.

Hesabu 18:23 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Walawi wafanya kazi inayohusiana na hema ya kukutania. Wataajibika kwa dhambi inyohusiana na hema. Hii itakuwa sheri ya kudumu kwa watu wote wa uzao wako. Na miongoni mwa watu wa Israeli hawa hawatakuwa na urithi.

Hesabu 18:24 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa kuwa zaka za wana wa Israeli, wanazotoa kama mchango kwangu -ndivyo hivyo ambavyo nimewapa Walawi kuwa urithi wao. Hiyo ndiyo sababu ya kuwaambia, Kuwa hawatakuwa na urithi kati ya watu wa Israeli.

Hesabu 18:26 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
“Inakupasa ukaseme na Walawi uwaambie, 'Mnapopokea zaka toka kwa watu ambayo BWANA amewapa kutoka kwao kuwa urithi, ndipo na nyie mtakapotoa sehemu ya kumi ya zaka hizo.

Hesabu 18:27 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Zaka yenu itahesabika kama moja ya mapato ya sakafu ya kupuria nafaka ya mazao yenu au mazao ya vinu vya kukamulia zabibu.

Hesabu 18:28 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa hiyo na ninyi lazima mtoe mchango wenu kwa BWANA kutokana na zaka mnazopata kutoka kwa watu wa Israeli. Kutokana na hizo mtatoa matoleo yenu kwa Haruni yule kuhani.

Hesabu 18:29 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa kila sadaka mnayopata, mtatoa matoleo yenu kwa BWANA. Mtafanya hivi kutokana na vitu vizuri na vitakatifu sana ambavyo mmepewa.

Hesabu 18:30 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa hiyo utawaambia, 'Mnapotoa hayo matoleo mazuri, ndipo itahesabika kwa Walawi kuwa ni mazao yao kutoka kwenye sakafu za kupuria na vinu vyao vya kukamulia.

Hesabu 18:31 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ndipo matakapokula nafaka zote zinazobaki mahali popote, ninyi na famailia zenu kwa sababu ndiyo malipo yenu ya kazi y a kwenye hema ya kukutania.

Hesabu 18:32 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hamtakuwa na hatia yeyote kwa kuvila na kuvinywa, kama mtatoa kwa BWANA matoleo yenu mazuri mliyopokea. Lakini msizinajisi sadaka takatifu za wana wa Israeli, vinginevyo mtakufa.,”
Previous Chapter
« Hesabu 17 (SWHULB)
Next Chapter
Hesabu 19 (SWHULB) »

Available Bible Translations

American Standard Version
Numbers 18 (ASV) »
King James Version
Numbers 18 (KJV) »
GOD’S WORD® (GW)
Numbers 18 (GW) »
World English Bible
Numbers 18 (WEB) »
Louis Segond 1910
Nombres 18 (LSG) »
Luther Bibel 1912
Numeri 18 (LUTH1912) »
इंडियन रिवाइज्ड वर्जन - हिंदी
गिनती 18 (HINIRV) »
ਭਾਰਤੀ ਸੋਧਿਆ ਹੋਇਆ ਸੰਸਕਰਣ - ਪੰਜਾਬੀ
ਗਿਣਤੀ 18 (PANIRV) »
ভারতীয় সংশোধিত সংস্করণ - বাংলা
গননা 18 (BENIRV) »
இந்தியன் ரீவைஸ்டு வேர்ஷன் - தமிழ்
எண்ணாகமம் 18 (TAMIRV) »
इंडियन रिवाइज्ड वर्जन - मराठी
गणना 18 (MARIRV) »
ఇండియన్ రేవిజ్డ్ వెర్షన్ - తెలుగు
సంఖ్యాకాండం 18 (TELIRV) »
ઇન્ડિયન રિવાયઝ્ડ વર્ઝન - ગુજરાતી
ગણના 18 (GUJIRV) »
ಭಾರತೀಯ ಪರಿಷ್ಕೃತ ಆವೃತ್ತಿ - ಕನ್ನಡ
ಅರಣ್ಯಕಾಂಡ 18 (KANIRV) »
الكتاب المقدس باللغة العربية، فان دايك
اَلْعَدَد 18 (AVD) »
תנ ך עברי מודרני
במדבר 18 (HEB) »
Bíblia Sagrada Português
Números 18 (BSL) »
Kinh Thánh: Tiếng Việt
Dân Số 18 (VIE) »
Reina Valera Antigua
Números 18 (RVA) »
La Sacra Bibbia
Numeri 18 (RIV) »
圣 经 简体中文和合本
民 数 记 18 (CUVS) »
聖 經 繁體中文和合本
民 數 記 18 (CUVT) »
Bibla e Shenjtë
Numrat 18 (ALB) »
Svenska Bibeln 1917
4 Mosebok 18 (SV1917) »
Библия на русском
Числа 18 (RUSV) »
Українська Біблія
Числа 18 (UKR) »
Szent Biblia - Magyar
4 Mózes 18 (KAR) »
Българска Библия
Числа 18 (BULG) »
聖書 日本語
民数記 18 (JPN) »
Kitaabka Quduuska Ah
Tirintii 18 (SOM) »
De Heilige Schrift
Numberi 18 (NLD) »

Hesabu (SWHULB) Chapter Selection

SWHULB Book Selection List