Hesabu Chapter 16 SWHULB Bible Verse Images

Hesabu 16 Bible Verse Pictures. Choose from a large collection of inspirational, motivational and encouraging Bible verses with pictures of nature. Download and share Hesabu 16 inspirational Bible verse images. Bible verse pictures were created based on verses from the Swahili Unlocked Literal Bible (SWHULB). The Holy Bible in the Swahili language, Unlocked Literal Bible version.

Copyright © 2019 Door43 World Missions Community
Language: Kiswahili (Swahili)
Translation by: Door43 World Missions Community

Contributors: Alfred Danjuma, Bariki Malisa, Christina Abraham Kileo, Cloud Roman, Daniel Marura Chacha, Dina Mast, Dina Roman, Donald Shadarck Dutuyi, Emmanuel Masanja Mbaaga, Emmanuel Nyamalya, Erasmus Peter Malelo, Ev. Lazaro Chalomhola, Ezekiel Manala, Fred, Gabriel Gidale Merus, Gabriel Lwitakubi Mazige, James Makula, James Semnkai, Jeremiah Masasi, Jesse Katabi Masolwa, John Ojasi, Joyce Gilbert Masasi, Karen Riecks, Kazwanomo, Kennedy, Ker, Lameck Yakobo Tobotobo, Laurent Petro Malelo, Lazarus David Chalomhola, Makene Mafwele, Marco Luma Mahushi, Mathew Nkusa, Mathias William, Mr. James Semnkai .It., Musa Isaya Majama, Musa Luzali, Pastor John Kerim, Pastor Jordan, Philipo Mussa Kanwelle, Raphael Musa, Rev. Charles Mabisa, Rev. Yohana Batano, Robert Ndalahwa, Sadiki Kulwa, Samson Nungwana, Thobias Kazwanomo, Yohana Dutuyi, Yohana Magera, Zelote Loilang'akaki Lukumay, Rev. Erasmus Peter Malelo, Ev. Mathew Kazimoto, Rev. Dr. David Magoke, Rev. Elias Ndema, Rev. Alex Nyuri, Rev. Gungutu Elias, Rev. Lameck Tobotobo, Rev. Catherin D. Matia, Rev. Yohana S Dutuyi, Rev. Donald Dutuyi, GS. Andrew Gewe, Ev. Ezekiel Daudi, Rev. John Ndaluka, Ev. Moses Malugu, Rev. Moses Eliakim Ndege, Past. Isack A. Gomugo, Past. Mathias William, Rev. Yekonia M. Koko, Rev. Elisande Mhanga, Ev. James A. Makula.

This translation is made available to you under the terms of the Creative Commons Attribution Share-Alike license 4.0.

You have permission to share and redistribute this Bible translation in any format and to make reasonable revisions and adaptations of this translation, provided that:

  • You include the above copyright and source information.
  • If you make any changes to the text, you must indicate that you did so in a way that makes it clear that the original licensor is not necessarily endorsing your changes.
  • If you redistribute this text, you must distribute your contributions under the same license as the original.

Credits: In addition, we would like to give very special thanks to eBible.org for making Swahili Unlocked Literal Bible available in MySQL format.


Hesabu 16:1 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Sasa Kora mwana wa Izihari mwana wa Kohathi mwana wa Lawi, pamoja na Dathani na Abiramu mwana wa Eliabu, na Oni mwana wa Peleti, wa uzao wa Reubeni, waliwakusanya wanaume kadhaa.

Hesabu 16:2 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakamwinukia Musa, pamoja na wanaume fulani kutoka wana wa Israeli, viongozi wa watu wapatao mia mbili na hamsini waliokuwa wakifahamika katika ile jamii.

Hesabu 16:3 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Walikusanyika pamoja kumpinga Musa na Haruni. Wakawaambia, “Ninyi sasa mnatumia mamlaka zaidi ya uwezo wenu! Watu wote wamejitenga, kila mmoja wao, na BWANA yuko pamoja nao. Kwa nini mnajiinua sana juu ya watu wengine wa BWANA?”

Hesabu 16:4 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Musa alipoyasikia hayo, akalala kifudifudi.

Hesabu 16:5 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akamwambia Kora na wote aliokuwa nao, “Asubuhi BWANA atafanya ijulikane ni nani walio wake na nani aliyetengwa kwa ajili yake. Atamleta huyo mtu karibu na yeye. Yule anayemchagua atamleta karibu naye.

Hesabu 16:6 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Fanya hivi, wewe Kora na kundi lako.

Hesabu 16:7 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kesho mchukue vyetezo na muweke moto na ubani ndani yake mbele ya BWANA. Yule ambaye BWANA amemchagua, atamtenga kwa BWANA. Sasa imetosha ninyi watu wa uzao wa Lawi,”

Hesabu 16:8 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Tena Musa akamwambia Kora, “Sasa unisililize, ninyi watu wa uzao wa Lawi:

Hesabu 16:9 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Je ni jambo dogo kwenu kwamba Mngu wa mbinguni amewatenga ninyi kutoka watu wa Israeli, ili awalete ninyi karibu na yeye, ili mfanye kazi katika masikani ya BWANA na kusimama mbele ya watu ili muwatumikie?

Hesabu 16:10 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Amewasogeza karibu, na ndugu zako, wa uzao wa Lawi pamoja nanyi, na sasa mnataka na ukuhani pia!

Hesabu 16:11 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hiyo ndiyo sababu wewe na kundi lako mmekusanyika pamoja kinyume na BWANA. Kwa nini mnalalamika juu ya Haruni, ambaye anamtii BWANA?”

Hesabu 16:12 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha Musa akamwita Dathani na Abiramu, wana wa Eliabu, lakini wakasema, “hatutakuja.

Hesabu 16:13 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwani jambo dogo kwamba umetuleta mpaka kwenye nchi inayotiririka maziwa na asali, ili kutuua katika jangwa hili? Sasa unataka kujifanya kuwa mtawala wetu!

Hesabu 16:14 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Na kwa nyongeza, haujatuingiza kwenye nchi ya kutiririka maziwa na asali, au kutupa urithi wa mashamba na mashamba ya mizabibu. Sasa unataka kutupofusha na ahadi hewa? Hatutakuja kwako.”

Hesabu 16:15 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Musa alikasirika sana na akamwambia BWANA, “Usisipokee sadaka zao. Sijachukua punda mmoja kutoka kwao, na sijamdhuru hata mmoja wao.”

Hesabu 16:16 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha Musa akamwambia Kora, “Kesho wewe na kundi lako mtaenda mbele za BWANA-wewe na wao na Haruni.

Hesabu 16:17 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kila mmoja wenu atatwaa chetezo na kuweka ubani ndani yake. Ndipo kila mtu atamletea BWANA chetezo chake, vyetezo mia mbili na hamsini. Wewe na Haruni, pia, kila mmoja ataleta chetezo chake.

Hesabu 16:18 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa hiyo kila mtu alitwaa chetezo chake, akaweka moto ndani yake, akaweka na ubani ndani yake, na kusimama mbele ya lango la hema ya kukutania pamoja na Musa na Haruni.

Hesabu 16:19 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kora naye akawakusanya watu wote waliokuwa kinyume na Musa na Haruni hapo kwenye lango la hema ya kukutania, na kisha utukufu wa BWANA ukaonekana kwa watu wote.

Hesabu 16:20 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ndipo BWANA aliposema na Musa na Haruni:

Hesabu 16:21 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
“Tokeni ninyi kutoka hawa watu ili nipate kuwaangamiza haraka.”

Hesabu 16:22 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Musa na Haruni wakalala kifudifudi na kusema, “Mungu, Mungu wa wote wenye mwili, kama mtu akitenda dhambi, ni lazima uwe na hasira na watu wote?”

Hesabu 16:24 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
“Sema na watu wote, uwaaambie, 'Tokeni kwenye hema ya Kora, Dathani, na Abiramu.'”

Hesabu 16:25 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha Musa akaamuka akaenda kwa Dathani na Kwa Abiramu; viongozi wa Israeli wakamfuata.

Hesabu 16:26 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akaongea na watu wote akasema, “Sasa jitengeni na hema ya hawa watu waovu na msiguse kitu chochote kilicho chao, vinginevyo mtaangamizwa na dhambi zao.”

Hesabu 16:27 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa hiyo watu wote toka pande zote za hema ya Kora, Dathani na Abiramu wakaondoka. Dathani na Abiramu wakatoka nje wakasimama kwenye lango la hema zao, wakiwa na wake wao, wana, na watoto wao.

Hesabu 16:28 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha Musa akasema, “Kwa hili sasa mtatambua kuwa BWANA amenituma kufanya kazi hizi zote, kwa kuwa sijazifanya kwa uwezo wangu.

Hesabu 16:29 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kama hawa watu watakufa kifo cha kawaida ambacho humpata kila mmoja, basi BWANA hakunituma.

Hesabu 16:30 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini kama BWANA aumbaye malango ya ardhi ambayo huwameza kama mdomo mkubwa, pamoja na familia zao, na kama wataingia ndani ya shimo wakiwa hai, ndipo mtakapojua kuwa wamemdharau BWANA,”

Hesabu 16:31 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mara ghafla Musa alipomaliza kusema maneno haya, aridhi ya pale walipokuwa ikafunguka.

Hesabu 16:32 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Dunia ikafungua makanwa yake na kuwameza, familia zao na watu wote wa Kora, pamoja na mali zao zote.

Hesabu 16:33 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wao na kila mmoja kwenye familia zao wakaingia ndani shimoni wakiwa hai. Dunia ikwafunika, na kwa njia hii wakapotea kutoka miongoni mwa ile jamii.

Hesabu 16:34 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Nao Israeli yote waliokuwa karibu nao wakakimbia kwa sababu ya vilio vyao. Walisema kwa mshangao, “Nchi isije kutumeza na sisi!”

Hesabu 16:35 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha moto ukashuka toka kwa BWANA na kuwaangamiza wale wanaume 250 waliokuwa wametoa ubani.

Hesabu 16:36 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Tena BWANA akanena na Musa, akasema,

Hesabu 16:37 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
“Mwambie Eliazari mwana wa Haruni yule kuhani achukue vile vyetezo kutoka ule moto, kwa kuwa vile vyetezo vimetengwa ka ajili yangu. Na aumwage ule moto mbali.

Hesabu 16:38 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Vitwae vile vyetezo vya wale waliopoteza maisha yao kwa sababu ya dhambi zao. Na vifanyike kuwa mbao za kufuliwa ili viwe vifuniko vya madhabahu. Kwa kuwa wale watu walivitoa kwangu, kwa hiyo ni vitakatifu. Vitakuwa ishara ya uwepo wangu kwa wana wa Israeli.”

Hesabu 16:39 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Naye Eleazari yule kuhani akavichukue vile vyetezo vya shaba ambavyo vilikuwa vimetumiwa na wale watu walioungua, na vikafuliwa kuwa vifuniko vya madhbahu,

Hesabu 16:40 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
ili kuwa ukumbusho kwa wana wa Israeli, ili kwamba asije akatokea mtu toka nje ya uzao wa Haruni akaja kutoa ubani kwa BWANA, ili wasije kuwa kama Kora na kundi lake— kama vile BWANA alivyoamuru kupitia kinywa cha Musa.

Hesabu 16:41 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini siku iliyofuata asubuhi watu wa Israeli wakamlalamikia Musa na Haruni. Nao walisema, “Umeua watu wa BWANA.”

Hesabu 16:42 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha ikatokea, wakati watu walipokuwa wamekusanyika kinyume na Musa na Haruni, wakatazama kuielekea hema ya kukutania, na tazama lile wingu lilikuwa likiifunika. Utukufu wa BWANA ukaonekana,

Hesabu 16:43 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Musa na Haruni wakaja mbele ya hema ya kukutania.

Hesabu 16:44 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha BWANA akanena na Musa, akamwambia,

Hesabu 16:45 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
“Toka kati ya watu hawa ili niwaangamize haraka.” Musa na Haruni wakalala chini kifudifudi.

Hesabu 16:46 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Musa akamwambia Haruni, uchukue chetezo, na utie ndani moto kutoka madhabahuni, tia na uvumba ndani yake, upeleke haraka kwa watu, na ukafanye upatanisho kwao, kwa sababu hasira hii inatoka kwa BWANA. Tauni imeanza.”

Hesabu 16:47 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa hiyo Haruni akafanya kama alivyoelekezwa na Musa. Akakimbia kati ya watu. na Tauni ilikuwa imeanza kuenea kati ya watu, kwa hiyo akaweka ndani yake uvumba na akafanya upatanisho wa watu.

Hesabu 16:48 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Haruni akasimama kati kati ya zile maiti na watu hai; na kwa njia hii ile tauni ikazuiwa.

Hesabu 16:49 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Idadi ya wale waliokuwa wamekufa kwa tauni walikuwa14, 000, nje na wale waliokufa kutokana na swala la Kora.

Hesabu 16:50 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Haruni akarudi kwa Musa kwenye lango la hema ya kukutania, na ile tauni ikakoma.
Previous Chapter
« Hesabu 15 (SWHULB)
Next Chapter
Hesabu 17 (SWHULB) »

Available Bible Translations

American Standard Version
Numbers 16 (ASV) »
King James Version
Numbers 16 (KJV) »
GOD’S WORD® (GW)
Numbers 16 (GW) »
World English Bible
Numbers 16 (WEB) »
Louis Segond 1910
Nombres 16 (LSG) »
Luther Bibel 1912
Numeri 16 (LUTH1912) »
इंडियन रिवाइज्ड वर्जन - हिंदी
गिनती 16 (HINIRV) »
ਭਾਰਤੀ ਸੋਧਿਆ ਹੋਇਆ ਸੰਸਕਰਣ - ਪੰਜਾਬੀ
ਗਿਣਤੀ 16 (PANIRV) »
ভারতীয় সংশোধিত সংস্করণ - বাংলা
গননা 16 (BENIRV) »
இந்தியன் ரீவைஸ்டு வேர்ஷன் - தமிழ்
எண்ணாகமம் 16 (TAMIRV) »
इंडियन रिवाइज्ड वर्जन - मराठी
गणना 16 (MARIRV) »
ఇండియన్ రేవిజ్డ్ వెర్షన్ - తెలుగు
సంఖ్యాకాండం 16 (TELIRV) »
ઇન્ડિયન રિવાયઝ્ડ વર્ઝન - ગુજરાતી
ગણના 16 (GUJIRV) »
ಭಾರತೀಯ ಪರಿಷ್ಕೃತ ಆವೃತ್ತಿ - ಕನ್ನಡ
ಅರಣ್ಯಕಾಂಡ 16 (KANIRV) »
الكتاب المقدس باللغة العربية، فان دايك
اَلْعَدَد 16 (AVD) »
תנ ך עברי מודרני
במדבר 16 (HEB) »
Bíblia Sagrada Português
Números 16 (BSL) »
Kinh Thánh: Tiếng Việt
Dân Số 16 (VIE) »
Reina Valera Antigua
Números 16 (RVA) »
La Sacra Bibbia
Numeri 16 (RIV) »
圣 经 简体中文和合本
民 数 记 16 (CUVS) »
聖 經 繁體中文和合本
民 數 記 16 (CUVT) »
Bibla e Shenjtë
Numrat 16 (ALB) »
Svenska Bibeln 1917
4 Mosebok 16 (SV1917) »
Библия на русском
Числа 16 (RUSV) »
Українська Біблія
Числа 16 (UKR) »
Szent Biblia - Magyar
4 Mózes 16 (KAR) »
Българска Библия
Числа 16 (BULG) »
聖書 日本語
民数記 16 (JPN) »
Kitaabka Quduuska Ah
Tirintii 16 (SOM) »
De Heilige Schrift
Numberi 16 (NLD) »

Hesabu (SWHULB) Chapter Selection

SWHULB Book Selection List