Mwanzo Chapter 19 SWHULB Bible Verse Images

Mwanzo 19 Bible Verse Pictures. Choose from a large collection of inspirational, motivational and encouraging Bible verses with pictures of nature. Download and share Mwanzo 19 inspirational Bible verse images. Bible verse pictures were created based on verses from the Swahili Unlocked Literal Bible (SWHULB). The Holy Bible in the Swahili language, Unlocked Literal Bible version.

Copyright © 2019 Door43 World Missions Community
Language: Kiswahili (Swahili)
Translation by: Door43 World Missions Community

Contributors: Alfred Danjuma, Bariki Malisa, Christina Abraham Kileo, Cloud Roman, Daniel Marura Chacha, Dina Mast, Dina Roman, Donald Shadarck Dutuyi, Emmanuel Masanja Mbaaga, Emmanuel Nyamalya, Erasmus Peter Malelo, Ev. Lazaro Chalomhola, Ezekiel Manala, Fred, Gabriel Gidale Merus, Gabriel Lwitakubi Mazige, James Makula, James Semnkai, Jeremiah Masasi, Jesse Katabi Masolwa, John Ojasi, Joyce Gilbert Masasi, Karen Riecks, Kazwanomo, Kennedy, Ker, Lameck Yakobo Tobotobo, Laurent Petro Malelo, Lazarus David Chalomhola, Makene Mafwele, Marco Luma Mahushi, Mathew Nkusa, Mathias William, Mr. James Semnkai .It., Musa Isaya Majama, Musa Luzali, Pastor John Kerim, Pastor Jordan, Philipo Mussa Kanwelle, Raphael Musa, Rev. Charles Mabisa, Rev. Yohana Batano, Robert Ndalahwa, Sadiki Kulwa, Samson Nungwana, Thobias Kazwanomo, Yohana Dutuyi, Yohana Magera, Zelote Loilang'akaki Lukumay, Rev. Erasmus Peter Malelo, Ev. Mathew Kazimoto, Rev. Dr. David Magoke, Rev. Elias Ndema, Rev. Alex Nyuri, Rev. Gungutu Elias, Rev. Lameck Tobotobo, Rev. Catherin D. Matia, Rev. Yohana S Dutuyi, Rev. Donald Dutuyi, GS. Andrew Gewe, Ev. Ezekiel Daudi, Rev. John Ndaluka, Ev. Moses Malugu, Rev. Moses Eliakim Ndege, Past. Isack A. Gomugo, Past. Mathias William, Rev. Yekonia M. Koko, Rev. Elisande Mhanga, Ev. James A. Makula.

This translation is made available to you under the terms of the Creative Commons Attribution Share-Alike license 4.0.

You have permission to share and redistribute this Bible translation in any format and to make reasonable revisions and adaptations of this translation, provided that:

  • You include the above copyright and source information.
  • If you make any changes to the text, you must indicate that you did so in a way that makes it clear that the original licensor is not necessarily endorsing your changes.
  • If you redistribute this text, you must distribute your contributions under the same license as the original.

Credits: In addition, we would like to give very special thanks to eBible.org for making Swahili Unlocked Literal Bible available in MySQL format.


Mwanzo 19:1 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Malaika wawili wakaja Sodoma jioni, wakati ambao Lutu alikuwa amekaa langoni mwa Sodoma. Lutu akawaona, akainuka kuwalaki, na akainama uso wake chini ardhini.

Mwanzo 19:2 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akasema, Tafadhari Bwana zangu, nawasihi mgeuke mwende kwenye nyumba ya mtumishi wenu, mlale pale usiku na muoshe miguu yenu. Kisha muamke asubuhi na mapema muondoke.” Nao wakasema, “Hapana, usiku tutalala mjini.”

Mwanzo 19:3 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini akawasihi sana, mwishowe wakaondoka pamoja nae, na wakaingia katika nyumba yake. Akaandaa chakula na kuoka mkate usiotiwa chachu, wakala.

Mwanzo 19:4 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini kabla hawaja lala, wanaume wa mji, wa Sodoma, vijana kwa wazee wakaizunguka nyumba, wanaume wote kutoka kila kona ya mji.

Mwanzo 19:5 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakamwita Lutu, na kumwambia, “Wale wanaume walioingia kwako usiku wakowapi? watoe hapa nje waje kwetu, ili tuweze kulala nao.”

Mwanzo 19:6 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lutu akatoka nje na akafunga mlango.

Mwanzo 19:7 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akasema, “Nawasihi, ndugu zangu, msitende uovu.

Mwanzo 19:8 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Tazama, nina mabinti wawili ambao hawajawahi kulala na mwanaume yeyote. Nawaomba tafadhari niwalete kwenu, na muwafanyie lolote muonalo kuwa jema machoni penu. Msitende lolote kwa wanaume hawa, kwa kuwa wamekuja chini ya kivuli cha dari yangu.”

Mwanzo 19:9 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakasema, “Ondoka hapa!” Wakasema pia, huyu alikuja kukaa hapa kama mgeni, na sasa amekuwa mwamuzi! Sasa tutakushugulilia vibaya wewe kuliko wao.” Wakamsonga sana huyo mtu, huyo Lutu, na wakakaribia kuvunja mlango.

Mwanzo 19:10 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini wale wanaume wakamkamata Lutu na kumweka ndani na wakafunga mlango.

Mwanzo 19:11 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha wale wageni wa Lutu wakawapiga kwa upofu wale wanaume waliokuwa nje ya nyumba, vijana na wazee kwa pamoja, kiasi kwamba wakachoka wakati wakiutafuta mlango.

Mwanzo 19:12 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Basi wale watu wakamwambia Lutu, Je una mtu mwingine yeyote hapa? wakwe zako, wanao na mabinti zako, na yeyote mwingine katika huu mji, ukawatoe hapa.

Mwanzo 19:13 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa kuwa tunakaribia kuiangamiza sehemu hii, kwa sababu mashitaka dhidi yake mbele ya Yahwe yamezidi kiasi kwamba ametutuma kuuangamiza.”

Mwanzo 19:14 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lutu akatoka na akazungumza na wakwe zake, wanaume ambao walikuwa wamewaposa binti zake, akawambia, “Ondokeni upesi mahali hapa, kwa kuwa Yahwe anakaribia kuuangamiza mji.” Lakini kwa wakwe zake alionekana kuwa anawatania.

Mwanzo 19:15 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Alfajiri, malaika wakamsihi Lutu, wakisema, ondoka, mtwae mkeo na binti zako wawili ambao wako hapa, ili kwamba usipotelee katika adhabu ya mji huu.”

Mwanzo 19:16 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini akakawia-kawia. Kwa hiyo watu wale wakamshika mkono wake, na mkono wa mkewe, na mikono ya binti zake wawili, kwa sababu Yahwe alimhurumia. Wakawatoa nje, na kuwaweka nje ya mji.

Mwanzo 19:17 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakisha kuwatoa nje mmoja wa wale watu akasema, “jiponye nafsi yako! usitazame nyuma, au usikae mahali popote kwenye hili bonde. Toroka uende milimani ili kwamba usije ukatoweshwa mbali.”

Mwanzo 19:18 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lutu akawambia, “Hapana, tafadhali bwana zangu!

Mwanzo 19:19 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mtumishi wenu amepata kibali machoni pako, na umenionesha wema ulio mkuu kwa kuokoa maisha yangu, lakini sitaweza kutorokea milimani, kwa sababu mabaya yataniwahi na nitakufa.

Mwanzo 19:20 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Tazama, ule mji pale uko karibu nijisalimishe pale, na ni mdogo. Tafadhari niacheni nikimbilie pale ( Je Siyo mdogo ule?), na maisha yangu yataokolewa.”

Mwanzo 19:21 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akamwambia, “Sawa, nimekubali ombi hili pia, kwamba sitaangamiza mji ambaoumeutaja.

Mwanzo 19:22 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Harakisha! toroka uende pale, kwa kuwa sitafanya chochote mpaka ufike pale.” kwa hiyo mji ule ukaitwa Soari.

Mwanzo 19:23 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Jua lilikuwa limekwisha chomoza juu ya nchi wakati Lutu alipofika Soari.

Mwanzo 19:24 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kisha Yahwe akanyesha juu ya Sodoma na Gomora kiberiti na moto toka kwa Yahwe mbinguni.

Mwanzo 19:25 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akaharibu miji ile, na bonde lote, na vyote vilivyomo katika miji, na mimea iliyo chipua juu ya ardhi.

Mwanzo 19:26 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini mke wa Lutu aliye kuwa nyuma yake, akatazama nyuma, na akawa nguzo ya chumvi.

Mwanzo 19:27 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Abraham akaamuka asubuhi na mapema akaenda mahali alipokuwa amesimama mbele ya Yahwe.

Mwanzo 19:28 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akatazama chini kuelekea Sodoma na Gomora na kuelekea katika nchi yote bondeni. Akaona na tazama, moshi ulikuwauki ukienda juu kutoka chini kama moshi wa tanuru.

Mwanzo 19:29 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakati Mungu alipoharibu miji ya bondeni, Mungu akamkumbuka Abraham. Akamtoa Lutu kutoka katika maangamizi alipoangamiza miji ambayo katika hiyo Lutu aliishi.

Mwanzo 19:30 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini Lutu akapanda juu kutoka Soari na kwenda kuishi katika milima akiwa pamoja na binti zake wawili, kwa sababu aliogopa kuishi Soari. Kwa hiyo akaishi pangoni, yeye na binti zake wawili.

Mwanzo 19:31 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yule wa kwanza akamwambia yule mdogo, “Baba yetu ni mzee, na hakuna mwanaume mahali popote wa kulala na sisi kulingana na desturi ya dunia yote.

Mwanzo 19:32 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Njoo na tumnyweshe baba yetu mvinyo na tulale naye ili kwamba tuendeleze uzao wa baba yetu.”

Mwanzo 19:33 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa hiyo wakamnywesha baba yako mvinyo usiku ule. Kisha yule wa kwanza akaingia na akalala na baba yake; Baba yake hakujua ni wakati gani alikuja kulala, wala wakati alipo amka.

Mwanzo 19:34 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Siku iliyo fuata yule wa kwanza akamwambia mdogowake, “Sikiliza, usiku wa jana nililala na baba yangu. Na tumnyweshe mvinyo usiku wa leo pia, na uingie ukalale naye. Ili kwamba tuendeleze uzao wa baba yetu.”

Mwanzo 19:35 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa hiyo wakamnywesha baba yao mvinyo usiku ule pia, na yule mdogo akaenda na akalala naye. Baba yake hakujua ni wakati gani alilala, wala wakati alipoamka.

Mwanzo 19:36 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Basi hao binti wote wawili wa Lutu wakapata mimba kwa baba yao.

Mwanzo 19:37 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wa kwanza akazaa mwana wa kiume, na akamwita jina lake Moabu. Akawa ndiye baba wa wamoabu hata leo.

Mwanzo 19:38 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Nayule mdogo naye akazaa mwana wa kiume, na akamwita Benami. Huyu ndiye baba wa watu wa Waamoni hata leo.
Previous Chapter
« Mwanzo 18 (SWHULB)
Next Chapter
Mwanzo 20 (SWHULB) »

Available Bible Translations

American Standard Version
Genesis 19 (ASV) »
King James Version
Genesis 19 (KJV) »
GOD’S WORD® (GW)
Genesis 19 (GW) »
World English Bible
Genesis 19 (WEB) »
Louis Segond 1910
Genèse 19 (LSG) »
Luther Bibel 1912
Genesis 19 (LUTH1912) »
इंडियन रिवाइज्ड वर्जन - हिंदी
उत्पत्ति 19 (HINIRV) »
ਭਾਰਤੀ ਸੋਧਿਆ ਹੋਇਆ ਸੰਸਕਰਣ - ਪੰਜਾਬੀ
ਪੈਦਾਇਸ਼ 19 (PANIRV) »
ভারতীয় সংশোধিত সংস্করণ - বাংলা
আদি 19 (BENIRV) »
இந்தியன் ரீவைஸ்டு வேர்ஷன் - தமிழ்
ஆதியாகமம் 19 (TAMIRV) »
इंडियन रिवाइज्ड वर्जन - मराठी
उत्पत्ति 19 (MARIRV) »
ఇండియన్ రేవిజ్డ్ వెర్షన్ - తెలుగు
ఆదికాండం 19 (TELIRV) »
ઇન્ડિયન રિવાયઝ્ડ વર્ઝન - ગુજરાતી
ઉત્પત્તિ 19 (GUJIRV) »
ಭಾರತೀಯ ಪರಿಷ್ಕೃತ ಆವೃತ್ತಿ - ಕನ್ನಡ
ಆದಿಕಾಂಡ 19 (KANIRV) »
الكتاب المقدس باللغة العربية، فان دايك
اَلتَّكْوِينُ 19 (AVD) »
תנ ך עברי מודרני
בראשית 19 (HEB) »
Bíblia Sagrada Português
Gênesis 19 (BSL) »
Kinh Thánh: Tiếng Việt
Sáng Thế 19 (VIE) »
Reina Valera Antigua
Génesis 19 (RVA) »
La Sacra Bibbia
Genesi 19 (RIV) »
圣 经 简体中文和合本
创 世 纪 19 (CUVS) »
聖 經 繁體中文和合本
創 世 記 19 (CUVT) »
Bibla e Shenjtë
Zanafilla 19 (ALB) »
Svenska Bibeln 1917
1 Mosebok 19 (SV1917) »
Библия на русском
Бытие 19 (RUSV) »
Українська Біблія
Буття 19 (UKR) »
Szent Biblia - Magyar
1 Mózes 19 (KAR) »
Българска Библия
Битие 19 (BULG) »
聖書 日本語
創世記 19 (JPN) »
Kitaabka Quduuska Ah
Bilowgii 19 (SOM) »
De Heilige Schrift
Genesis 19 (NLD) »

Mwanzo (SWHULB) Chapter Selection

SWHULB Book Selection List