Mwanzo Chapter 34 SWHULB Bible Verse Images

Mwanzo 34 Bible Verse Pictures. Choose from a large collection of inspirational, motivational and encouraging Bible verses with pictures of nature. Download and share Mwanzo 34 inspirational Bible verse images. Bible verse pictures were created based on verses from the Swahili Unlocked Literal Bible (SWHULB). The Holy Bible in the Swahili language, Unlocked Literal Bible version.

Copyright © 2019 Door43 World Missions Community
Language: Kiswahili (Swahili)
Translation by: Door43 World Missions Community

Contributors: Alfred Danjuma, Bariki Malisa, Christina Abraham Kileo, Cloud Roman, Daniel Marura Chacha, Dina Mast, Dina Roman, Donald Shadarck Dutuyi, Emmanuel Masanja Mbaaga, Emmanuel Nyamalya, Erasmus Peter Malelo, Ev. Lazaro Chalomhola, Ezekiel Manala, Fred, Gabriel Gidale Merus, Gabriel Lwitakubi Mazige, James Makula, James Semnkai, Jeremiah Masasi, Jesse Katabi Masolwa, John Ojasi, Joyce Gilbert Masasi, Karen Riecks, Kazwanomo, Kennedy, Ker, Lameck Yakobo Tobotobo, Laurent Petro Malelo, Lazarus David Chalomhola, Makene Mafwele, Marco Luma Mahushi, Mathew Nkusa, Mathias William, Mr. James Semnkai .It., Musa Isaya Majama, Musa Luzali, Pastor John Kerim, Pastor Jordan, Philipo Mussa Kanwelle, Raphael Musa, Rev. Charles Mabisa, Rev. Yohana Batano, Robert Ndalahwa, Sadiki Kulwa, Samson Nungwana, Thobias Kazwanomo, Yohana Dutuyi, Yohana Magera, Zelote Loilang'akaki Lukumay, Rev. Erasmus Peter Malelo, Ev. Mathew Kazimoto, Rev. Dr. David Magoke, Rev. Elias Ndema, Rev. Alex Nyuri, Rev. Gungutu Elias, Rev. Lameck Tobotobo, Rev. Catherin D. Matia, Rev. Yohana S Dutuyi, Rev. Donald Dutuyi, GS. Andrew Gewe, Ev. Ezekiel Daudi, Rev. John Ndaluka, Ev. Moses Malugu, Rev. Moses Eliakim Ndege, Past. Isack A. Gomugo, Past. Mathias William, Rev. Yekonia M. Koko, Rev. Elisande Mhanga, Ev. James A. Makula.

This translation is made available to you under the terms of the Creative Commons Attribution Share-Alike license 4.0.

You have permission to share and redistribute this Bible translation in any format and to make reasonable revisions and adaptations of this translation, provided that:

  • You include the above copyright and source information.
  • If you make any changes to the text, you must indicate that you did so in a way that makes it clear that the original licensor is not necessarily endorsing your changes.
  • If you redistribute this text, you must distribute your contributions under the same license as the original.

Credits: In addition, we would like to give very special thanks to eBible.org for making Swahili Unlocked Literal Bible available in MySQL format.


Mwanzo 34:1 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Basi Dina, Binti wa Lea aliyemzalia Yakobo, akaenda kuwaona wasichana wa nchi.

Mwanzo 34:2 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Shekemu mwana wa Hamori Mhivi, mwana mfalme wa nchi, akamwona na akamkamata kwa nguvu na kulala naye.

Mwanzo 34:3 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Akavutiwa na Dina, binti Yakobo. Akampenda msichana na kuongea naye kwa upole.

Mwanzo 34:4 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Shekemu akamwambia Hamori baba yeke, kusema, “Nipe msichana huyu kuwa mke wangu.”

Mwanzo 34:5 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Basi Yakobo akasikia kwamba alikuwa amemchafua Dina binti yake. Wanawe walikuwa pamoja na wanyama uwandani, hivyo Yakaobo akawangoja hata walipokuja.

Mwanzo 34:6 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hamori baba wa Shekemu akaenda kuongea na Yakobo.

Mwanzo 34:7 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wana wa Yakobo waliposikia neno hili wakaja kutoka uwandani. Watu hawa walichukizwa sana. Walikasirika sana kwa sababu alikuwa amemwaibisha Israeli kwa kumlazimisha binti wa Yakobo, kwa maana jambo kama hilo halikupasa kutendeka.

Mwanzo 34:8 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hamori akaongea nao, akisema, “Shekemu mwanangu anampenda binti yenu. Tafadhari mpeni kuwa mke wake.

Mwanzo 34:9 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mwoane nasi, tupeni binti zenu, na mjichukulie binti zetu kwa ajili yenu wenyewe.

Mwanzo 34:10 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Mtaishi nasi, na nchi itakuwa wazi kwa ajili yenu kufanya biashara humo, na kupata mali.”

Mwanzo 34:11 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Shekemu akamwambia baba yake na ndugu zake, “Na nione kibari machoni penu, na chochote mtakachoniambia nitatoa.

Mwanzo 34:12 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Niambieni kiasi kikubwa chochote cha mahari na zawadi kama mtakavyo, nami nitatoa chochote msemacho, lakini mnipe msichana kuwa mke wangu.”

Mwanzo 34:13 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wana wa Yakobo wakamjibu Shekemu na Hamori baba yake kwa hila, kwa sababu Shekemu alikuwa amemnajisi Dina dada yao.

Mwanzo 34:14 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakawambia, “Hatuwezi kufanya jambo hili, kumpa dada yetu mtu yeyote ambaye hajatailiwa; kwani hiyo ni aibu kwetu.

Mwanzo 34:15 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa sharti hili peke yake tutakubaliana nanyi: iwapo mtatailiwa kama sisi, ikiwa kila mtu mme miongoni mwenu atatailiwa.

Mwanzo 34:16 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Ndipo tutakapowapa binti zetu, nasi tutachukua binti zenu kwetu sisi wenyewe, na tutaishi nanyi na kuwa wamoja.

Mwanzo 34:17 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini kama hamtusikilizi na kutailiwa, ndipo tutakapomchukua dada yetu na kuondoka.

Mwanzo 34:18 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Maneno yao yakawafurahisha Hamori na Shekemu mwanaye.

Mwanzo 34:19 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kijana hakukawia kufanya walichokisema, kwa maana alipendezwa na binti Yakobo, na kwa sababu alikuwa mtu aliyeheshimiwa sana katika nyumba ya babaye.

Mwanzo 34:20 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Hamori na Shekemu mwanaye wakaenda katika lango la mji wao na kuongea na watu wa mji, kusema,

Mwanzo 34:21 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
“Watu hawa wanaamani nasi, hivyo na waishi katika nchi na kufanya biashara humo kwa maana, kweli, nchi ni kubwa ya kuwatosha. Haya na tuwachukue binti zao kuwa wake, nasi tuwape binti zetu.

Mwanzo 34:22 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Kwa shariti hili pekee watu hawa wanakubali kuishi nasi na kuwa wamoja: ikiwa kila mwanamme miongoni mwetu atatailiwa, kama wao.

Mwanzo 34:23 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Je wanyama wao na vitu vyao - wanyama wao wote kuwa wetu? Haya na tukubaliane nao, nao wataishi kati yetu.”

Mwanzo 34:24 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Watu wote wa mji wakamsikiliza Hamori na Shekemu, mwanaye. Kila mwanamme akatailiwa.

Mwanzo 34:25 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Katika siku ya tatu, walipokuwa katika maumivu bado, wawili wa wana wa Yakobo (Simoni na Lawi, kaka zake Dina), wakachukua kila mmoja upanga wake na kuushambulia mji ambao ulikuwa na uhakika wa ulinzi wake, nao wakauwa wanamme wote.

Mwanzo 34:26 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakamwua Hamori na Shekemu kwa makali ya upanga. Wakamchukua Dina kutoka nyumba ya Shekemu na kuondoka.

Mwanzo 34:27 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wale wana wengine wa Yakobo wakaja kwa maiti na kuuteka nyara mji, kwa sababu watu wale walikuwa wamemnajisi dada yao.

Mwanzo 34:28 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Wakachukua makundi yao ya kondoo, mbuzi, punda, na kila kitu ndani ya mji na viunga vyake

Mwanzo 34:29 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
utajiri wote. Watoto na wake zao wote, wakawachukua. Hata wakachukua kila kitu kilichokua katika nyumba.

Mwanzo 34:30 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Yakobo akawambia Simoni na Lawi, “Mmeleta shida juu yangu, kunifanya ninuke kwa wenyeji wa nchi, Wakanaani na Waperizi. Mimi nina watu wachache. Ikiwa watajikusanya pamoja kinyume changu na kunishambulia.”

Mwanzo 34:31 (SWHULB)
Square Portrait Landscape 4K UHD
Lakini Simoni na Lawi wakasema, “Je Shekemu alipaswa kumtendea dada yetu kama kahaba?”
Previous Chapter
« Mwanzo 33 (SWHULB)
Next Chapter
Mwanzo 35 (SWHULB) »

Available Bible Translations

American Standard Version
Genesis 34 (ASV) »
King James Version
Genesis 34 (KJV) »
GOD’S WORD® (GW)
Genesis 34 (GW) »
World English Bible
Genesis 34 (WEB) »
Louis Segond 1910
Genèse 34 (LSG) »
Luther Bibel 1912
Genesis 34 (LUTH1912) »
इंडियन रिवाइज्ड वर्जन - हिंदी
उत्पत्ति 34 (HINIRV) »
ਭਾਰਤੀ ਸੋਧਿਆ ਹੋਇਆ ਸੰਸਕਰਣ - ਪੰਜਾਬੀ
ਪੈਦਾਇਸ਼ 34 (PANIRV) »
ভারতীয় সংশোধিত সংস্করণ - বাংলা
আদি 34 (BENIRV) »
இந்தியன் ரீவைஸ்டு வேர்ஷன் - தமிழ்
ஆதியாகமம் 34 (TAMIRV) »
इंडियन रिवाइज्ड वर्जन - मराठी
उत्पत्ति 34 (MARIRV) »
ఇండియన్ రేవిజ్డ్ వెర్షన్ - తెలుగు
ఆదికాండం 34 (TELIRV) »
ઇન્ડિયન રિવાયઝ્ડ વર્ઝન - ગુજરાતી
ઉત્પત્તિ 34 (GUJIRV) »
ಭಾರತೀಯ ಪರಿಷ್ಕೃತ ಆವೃತ್ತಿ - ಕನ್ನಡ
ಆದಿಕಾಂಡ 34 (KANIRV) »
الكتاب المقدس باللغة العربية، فان دايك
اَلتَّكْوِينُ 34 (AVD) »
תנ ך עברי מודרני
בראשית 34 (HEB) »
Bíblia Sagrada Português
Gênesis 34 (BSL) »
Kinh Thánh: Tiếng Việt
Sáng Thế 34 (VIE) »
Reina Valera Antigua
Génesis 34 (RVA) »
La Sacra Bibbia
Genesi 34 (RIV) »
圣 经 简体中文和合本
创 世 纪 34 (CUVS) »
聖 經 繁體中文和合本
創 世 記 34 (CUVT) »
Bibla e Shenjtë
Zanafilla 34 (ALB) »
Svenska Bibeln 1917
1 Mosebok 34 (SV1917) »
Библия на русском
Бытие 34 (RUSV) »
Українська Біблія
Буття 34 (UKR) »
Szent Biblia - Magyar
1 Mózes 34 (KAR) »
Българска Библия
Битие 34 (BULG) »
聖書 日本語
創世記 34 (JPN) »
Kitaabka Quduuska Ah
Bilowgii 34 (SOM) »
De Heilige Schrift
Genesis 34 (NLD) »

Mwanzo (SWHULB) Chapter Selection

SWHULB Book Selection List